{"id":7642,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/7642/?format=json","text_counter":305,"type":"speech","speaker_name":"Mr. Bett","speaker_title":"","speaker":{"id":157,"legal_name":"Franklin Kipng'etich Bett","slug":"franklin-bett"},"content":"Bw. Naibu Spika wa Muda, ninafahamu kwamba mvua imeleta taharuki katika sehemu ya Mombasa na kuharibu barabara. Ningetaka kulihakikishia Bunge hili kwamba jambo hilo limenifikia na nimeamuru maofisa wangu waziangalie barabara hizo. Muda si muda, nitakuwa na ripoti kuhusu Kaunti ya Mombasa."}