{"id":765328,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/765328/?format=json","text_counter":284,"type":"speech","speaker_name":"Hon. Chumel","speaker_title":"","speaker":{"id":318,"legal_name":"Samuel Chumel Moroto","slug":"samuel-moroto"},"content":"Wakati wazungu walichukua maeneo hayo makubwa, je, hakukuwa na wenye kuishi hapo mbeleni? Tunataka jibu kwa hilo swali kwanza. Ripoti ilisema tufuatilie jambo hilo na tuhakikishe kwamba suluhisho limepatikana. Wengine wetu tumepakana na Trans Nzoia na tunasikizana na wenyeji. Tunahitaji kufidiwa ili tukae kama wengine. Lakini polisi kutumia nguvu kupita kiasi na hatimaye kuua ng’ombe ni hatia."}