{"id":781346,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/781346/?format=json","text_counter":170,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Faki","speaker_title":"","speaker":{"id":13211,"legal_name":"Mohamed Faki Mwinyihaji","slug":"mohamed-faki-mwinyihaji-2"},"content":"Bw. Spika, neno ‘Harambee’ linalotumika katika Coat of Arms halihusiani kamwe na ‘ambe’ambaye anasemekana ni Mungu katika sehemu zingine za dunia. Kwa hivyo nakubaliana na uamuzi wa Kamati ya Haki, Maswala ya Sheria na Haki za Kibinadamu, kwamba ombi la ndugu Aluoch Polo Aluochier halina msingi na linafaa kutupiliwa mbali. Asante."}