{"id":794192,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/794192/?format=json","text_counter":910,"type":"speech","speaker_name":"Hon. Mwale","speaker_title":"","speaker":{"id":13311,"legal_name":"Nicholas Scott Tindi Mwale","slug":"nicholas-scott-tindi-mwale"},"content":"Kwa upande wa usalama, watalii wamekuwa wakisumbuliwa na magaidi. Mtalii mmoja alitekwa nyara na magaidi wakampeleka Somalia. Baadaye Serikali ilijaribu kumtafuta na baadaye Rais Kibaki aliyekuwa madarakani alituma wanajeshi Somalia kwa sababu ya huyo mgeni kutekwa nyara akiwa eneo la Pwani. Kwa hivyo Mswada huu utasaidia sana kuangalia vile eneo letu la Pwani na maziwa mengine yataangaliwa kiusalama."}