{"id":873847,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/873847/?format=json","text_counter":130,"type":"speech","speaker_name":"Nyali, Independent","speaker_title":"Hon. Mohamed Ali","speaker":{"id":13455,"legal_name":"Mohammed Ali Mohamed","slug":"mohamed-ali-mohamed"},"content":"Juzi nimeona kuna mgomo wa nesi. Wamesema kwamba hawalipwi vizuri na wataendelea kugoma. Mimi nawaunga mkono. Endeleeni kugoma mpaka siku ile mtaheshimiwa na muweze kuangaliwa, ili Wakenya waweze kuhudumiwa. Tangu hao manesi waanze kugoma, watu wengi wamefariki hospitalini. Hii si makosa ya mwanachi wa kawaida. Ni makosa ya Serikali. Madaktari Kenya nzima ni 11,000 kwa Wakenya milioni 45."}