{"id":873954,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/873954/?format=json","text_counter":237,"type":"speech","speaker_name":"Nominated, JP","speaker_title":"Hon. David ole Sankok","speaker":{"id":13166,"legal_name":"David Ole Sankok","slug":"david-ole-sankok"},"content":"Sio kawaida mtu kufariki katika hospitali ndogo ama zahanati kwa sababu wagonjwa wanaelekezwa katika hospitali ambazo zina vifaa. Lakini madaktari, kwa sababu ya kukosa kulipwa vizuri, wanajaribu hivi na vile katika hizo hospitali ndogo mpaka wagonjwa wanaaga dunia. Hoja hii itawafanya madaktari pia wawe waangalifu."}