{"id":875605,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/875605/?format=json","text_counter":349,"type":"speech","speaker_name":"Bahati, JP","speaker_title":"Hon. Onesmas Ngunjiri","speaker":{"id":1179,"legal_name":"Onesmas Kimani Ngunjiri","slug":"onesmas-kimani-ngunjiri"},"content":"Kwa hivyo, ningetaka kuomba Serikali yetu ichunguze na Waziri akisema jambo fulani litakuwa la bure, inatupasa kuangalia jambo hilo ili wasije wakawawekelea Wabunge mzigo ambao hawawezi. Katika maeneo mengine, watoto wanasimama darasani kwa sababu hawana viti. Hawana mahali pa kuketi na hata mawe hayapatikani bure. Yananunuliwa na hiyo pesa ya kununua hakuna. Haya ni mambo nyeti ambayo yanapaswa kuangaliwa."}