{"id":883649,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/883649/?format=json","text_counter":478,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Faki","speaker_title":"","speaker":{"id":13211,"legal_name":"Mohamed Faki Mwinyihaji","slug":"mohamed-faki-mwinyihaji-2"},"content":"Bi. Spika Wa Muda, sheria hii inatoa mwongozo kwa Executive na kuwapa uwezo wa kutunga kanuni; lakini lazima kanuni zitakazotungwa ziambatane na ile sheria iliyopitishwa. Haiwezekani kwamba sheria inazungumza tofauti na kanuni ambazo zinapitishwa na wale watekelezaji zinakuwa tofauti. Kwa hivyo, sheria inatoa mwongozo kwamba lazima kanuni zote zitakazotengenezwa zilingane na ile sheria iliyopitishwa."}