{"id":886060,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/886060/?format=json","text_counter":186,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Faki","speaker_title":"","speaker":{"id":13211,"legal_name":"Mohamed Faki Mwinyihaji","slug":"mohamed-faki-mwinyihaji-2"},"content":"pekee yake, itolewe kwa biashara za watu kibinafsi ambao walikuwa wanaleta mizigo hiyo Nairobi na kwingineko bila kushurutishwa na Serikali. Hivi ninavyoongea, ni kwamba shirika la Bandari la Kenya Ports Authority (KPA) wametoa arifa kwa waleta mizigo aina ya sukari, mchele, ngano na vinginevyo, kwamba hawana"}