{"id":895127,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/895127/?format=json","text_counter":334,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Faki","speaker_title":"","speaker":{"id":13211,"legal_name":"Mohamed Faki Mwinyihaji","slug":"mohamed-faki-mwinyihaji-2"},"content":"Asante, Bw. Spika wa Muda, kwa kunipa fursa hii kuchangia Hotuba ya Rais kwa Seneti na Bunge la Kitaifa. Kwanza ningependa kumpongeza Rais kwa Hotuba yake ambayo alilihakikishia Taifa kwamba nchi itaongozwa kwa sheria. Alikataa sheria kutumiwa vibaya na hiyo inamaanisha kwamba nchi itaendelea kuongozwa na Katiba yetu ambayo tulianzisha mwaka wa 2010."}