{"id":895149,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/895149/?format=json","text_counter":356,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Faki","speaker_title":"","speaker":{"id":13211,"legal_name":"Mohamed Faki Mwinyihaji","slug":"mohamed-faki-mwinyihaji-2"},"content":"Pia tukiangalia ukulima katika eneo la Mombasa, bado hakuna jambo lolote linalofanyika. Sehemu zingine watu wanapewa ruzuku za mbegu, mbolea na pembejeo nyingine lakini mpaka sasa katika eneo la Pwani au Mombasa, hakuna jambo lolote la ukulima ambalo linafanyika."}