{"id":895521,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/895521/?format=json","text_counter":39,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Boy","speaker_title":"","speaker":{"id":13200,"legal_name":"Issa Juma Boy","slug":"issa-juma-boy"},"content":"Ni jambo la kusikitisha sana hasa ukiona kwamba mwananchi amekubali kutoa ardhi yake kwa Serikali kujenga barabara. Leo watu hao ambao wametoa ardhi yao na hawajalipwa pesa zao wana familia na wanategemea kupata pesa hizo waweze kusaidia familia zao."}