{"id":895781,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/895781/?format=json","text_counter":299,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Madzayo","speaker_title":"","speaker":{"id":679,"legal_name":"Stewart Mwachiru Shadrack Madzayo","slug":"stewart-mwachiru-shadrack-madzayo"},"content":"Tunakumbuka ya kwamba mwaka wa 2017, hatimaye tu baada ya kupiga kura, kama Wakenya tulilumbana sana. Tulileta shida kubwa sana kwa sababu hatukukubali na tuliamini ya kwamba kura zetu katika National Super Alliance (NASA) ziliibiwa. Hatukukubali kabisa kwamba Serikali iliyoko katika mamlaka ilikuwa Serikali kamilifu iliyochaguliwa na Wakenya. Matokeo au mavuno yake ilikuwa fujo katika barabara na biashara na hali ya uchumi katika Kenya ikaenda chini."}