{"id":902797,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/902797/?format=json","text_counter":242,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Faki","speaker_title":"","speaker":{"id":13211,"legal_name":"Mohamed Faki Mwinyihaji","slug":"mohamed-faki-mwinyihaji-2"},"content":"Maseneta wote hapa wana tajriba ya kutosha kuwawezesha kukaa katika kamati yoyote na kuongoza katika nyadhifa zozote wanazopewa. Kwa hivyo, hatuna shaka kwamba watawasilisha maslahi yetu na maslahi ya kaunti zote katika Jamhuri ya Kenya kikamilifu. Sisi kama Seneti tutakubaliana na uamuzi wao."}