{"id":908991,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/908991/?format=json","text_counter":169,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Faki","speaker_title":"","speaker":{"id":13211,"legal_name":"Mohamed Faki Mwinyihaji","slug":"mohamed-faki-mwinyihaji-2"},"content":"Naunga mkono taarifa hii ili tuhakikishe Wakenya wanaweza kupata pasipoti kwa njia rahisi. Nafasi za kazi hapa Kenya ni adimu, kwa hivyo wengi wakiwa na pasipoti, wataweza kuenda kufanya kazi katika nchi zingine ili waweze kujielendesha kimaisha. Ikiwezekana, Kamati husika inafaa kutembelea ofisi za pasipoti ili wajionee shida zinazowakumba Wakenya."}