{"id":911849,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/911849/?format=json","text_counter":56,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Madzayo","speaker_title":"","speaker":{"id":679,"legal_name":"Stewart Mwachiru Shadrack Madzayo","slug":"stewart-mwachiru-shadrack-madzayo"},"content":"Bw. Spika, kuna vitengo vya ujasusi ambavyo vinaweza kuchunguza na kutuambia jinsi ya kuepuka janga kama hilo. Vitengo hivyo viko ndani ya serikali na watu hao wanalipwa mshahara. Ningependelea ya kwamba taarifa ya Sen. Farhiya ichukuliwe kwa umuhimu zaidi ili tupatiwe majibu mwafaka."}