{"id":918712,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/918712/?format=json","text_counter":242,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Wario","speaker_title":"","speaker":{"id":13224,"legal_name":"Golich Juma Wario","slug":"golich-juma-wario"},"content":"Ripoti hii ilirejeshwa katika Bunge zote mbili na ikajadiliwa na watu ambao wamesema sasa ni nzuri. Tuliposomewa Ripoti hiyo hapa mbele, tuliiona ikiwa nzuri kabisa. Nikiwa Mwanachama wa Kamati ya Ukulima, Ufugaji na Uvuvi, ambayo Mwenyekti wangu ni jirani hapa nyuma yangu, tuliweza kuikalia vizuri. Nilishiriki katika mazungumzo ya kuleta uwiano na tutaiunga mkono."}