{"id":922422,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/922422/?format=json","text_counter":88,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Wario","speaker_title":"","speaker":{"id":13224,"legal_name":"Golich Juma Wario","slug":"golich-juma-wario"},"content":"Asante, Bw. Spika, kunipa nafasi ili kumuunga mkono Seneta aliyewasilisha taarifa hii. Vile tunavyojua, kuna mambo yanayofanyika katika shule za upili. Kuna mambo yanayofanyika wanafunzi wanapojiunga na shule za upili na hiyo ni dhuluma. Kamati ya Elimu inafaa kufanya uchunguzi na kupendekeza jinsi ya kukomesha dhuluma katika shule za upili."}