{"id":922423,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/922423/?format=json","text_counter":89,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Wario","speaker_title":"","speaker":{"id":13224,"legal_name":"Golich Juma Wario","slug":"golich-juma-wario"},"content":"Wanafunzi wengi wanahofia kwenda shule kwa sababu kuna baadhi wanaoamrishwa kwenda kwa magoti. Baadhi humwagiwa maji baridi na wengine hupata kichapo cha mbwa. Hiyo si haki kwa sababu wazazi hupeleka watoto wao shuleni ili wasome bila shida. Ikiwa wanadhulumiwa, wengi hawawezi kusoma kwa sababu wanaogopa wenzao."}