{"id":922499,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/922499/?format=json","text_counter":165,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Wario","speaker_title":"","speaker":{"id":13224,"legal_name":"Golich Juma Wario","slug":"golich-juma-wario"},"content":"Bw. Spika, tunamheshimu sana Sen. (Dr.) Zani kutoka jimbo la Pwani, sehemu ile ya Kwale. Alitangulia kusema kwamba hatatumia neno “Bw. Spika” wala “mzungumzishi”. Hata hivyo, amemaliza kwa kutumia neon “mzungumzishi”. Tungependa aondoe arifa ambayo ametoa ili isikae katika rekodi zetu na kuheshimu Bunge la Seneti. Asante, Bw. Spika."}