{"id":92331,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/92331/?format=json","text_counter":102,"type":"speech","speaker_name":"Mr. Joho","speaker_title":"","speaker":{"id":30,"legal_name":"Hassan Ali Joho","slug":"hassan-joho"},"content":"Jambo la nidhamu, Bw. Naibu Spika. Mhe. Waziri Msaidizi amesema ikiwa kamati ya usalama ya wilaya yangu itapendekeza idadi fulani ya askari wanaohitajika katika eneo langu, basi yeye atawatuma askari hao. Ningependa Waziri Msaidizi atoe hakikisho katika Bunge hili kuwa kamati hiyo ikipendekeza idadi ya askari wanaohitajika katika eneo langu, atawatuma mara moja."}