{"id":925480,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/925480/?format=json","text_counter":129,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Wario","speaker_title":"","speaker":{"id":13224,"legal_name":"Golich Juma Wario","slug":"golich-juma-wario"},"content":"Ninaunga mkono taarifa hii ili kemikali na vitu vingine visiwekwe kwa nyama na hata vyakula vingine kama ndizi, machungwa na kadhalika. Chakula kiwekwe katika hali yake halisi ambayo imekuzwa katika mashamba ili tukuze jamii bora zenye afya."}