{"id":92764,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/92764/?format=json","text_counter":127,"type":"speech","speaker_name":"Mr. Ochiengâ","speaker_title":"","speaker":null,"content":"Bw. Naibu Spika, ningependa Waziri Msaidizi atuambie wana mipango gani kabambe ambayo itahakikisha kwamba watakuwa na magari na mafuta ya kutosha ili kwamba vijana ambao wameacha shule na hawajapata vitambulisho wapate kusajiliwa? Je, mpango huu utafanikishwa lini ili vijana hawa wapate kusajiliwa?"}