{"id":929381,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/929381/?format=json","text_counter":374,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Wario","speaker_title":"","speaker":{"id":13224,"legal_name":"Golich Juma Wario","slug":"golich-juma-wario"},"content":"Asante sana, Bi. Spika wa Muda, kwa kunipa nafasi hii ili nichangie Hoja iliyoletwa na Sen. Pareno. Kabla sijafanya hivyo, ningependa kutuma rambirambi zangu kwa jamaa na marafiki wa waliotuacha. Miongoni mwao ni marehemu mhe. Ken Okoth na aliyekuwa Gavana wa Bomet, mhe. Joyce Laboso. Tuko pamoja nao wakati huu mgumu."}