{"id":934612,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/934612/?format=json","text_counter":58,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Madzayo","speaker_title":"","speaker":{"id":679,"legal_name":"Stewart Mwachiru Shadrack Madzayo","slug":"stewart-mwachiru-shadrack-madzayo"},"content":"Asante, Bw. Spika wa Muda. Sheria zetu za mikataba ya Bunge la Seneti zinasema kwamba Mbunge anafaa kuvaa koti ambayo itakua imefika kwenye shingo na imeweza kumfunika kisawasawa. Hakuna mahali popote ambapo panasema kwamba mimi nimevaa hali sintofahamu ya kuingia ndani ya Bunge. Nataka kumwambia ndugu yangu, ambaye pia ni shemeji yangu, Sen. Linturi, kwamba vile nimevaa ni kadri na sheria za Bunge. Asante."}