{"id":939487,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/939487/?format=json","text_counter":300,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Faki","speaker_title":"","speaker":{"id":13211,"legal_name":"Mohamed Faki Mwinyihaji","slug":"mohamed-faki-mwinyihaji-2"},"content":"Kwa hivyo, Bi. Spika wa Muda, lazima tukemee vitisho vya Serikali kupunguza ruzuku kwa mahakama, na mawazo ya Serikali kwamba wanaweza kuendelea kujaribu kukwamisha utendakazi wa mahakama. Ni lazima tukemee upokonyaji wa uhuru wa mahakama, kwa sababu Uhuru huu utakapopokonywa, wananchi ndio watakuwa wanalalamika na kupoteza haki zao."}