{"id":945450,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/945450/?format=json","text_counter":209,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Faki","speaker_title":"","speaker":{"id":13211,"legal_name":"Mohamed Faki Mwinyihaji","slug":"mohamed-faki-mwinyihaji-2"},"content":"Ni heri tutumie fursa hii kuuza na kutangaza Kenya kama nchi ambayo ina amani na talanta tofautitofauti za kimichezo. Wengi huwa tunajulikana kwa mambo ambayo hatufai kuyataja kama vile ufisadi na mengine maovu ambayo hayafai katika jamii."}