{"id":945452,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/945452/?format=json","text_counter":211,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Faki","speaker_title":"","speaker":{"id":13211,"legal_name":"Mohamed Faki Mwinyihaji","slug":"mohamed-faki-mwinyihaji-2"},"content":"Nilipata fursa ya kuangalia mahojiano ya Cable News Network (CNN) na Eliud Kipchoge ambapo alisema kwamba hiyo nafasi ametwaa si kwamba yeye ndiyo bingwa. La! Lakini ameweza kuonyesha ulimwengu kwamba chochote ambacho binadamu anatumaini kufanya kwa urahisi. Ametoa changamoto kwa binadamu mwingine yeyote ulimwenguni ajaribu kupunguza muda wa 1:59.40. Amefutundisha kuwa yote yanawezekana tukiwa na imani."}