{"id":949200,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/949200/?format=json","text_counter":395,"type":"speech","speaker_name":"Lamu East, JP","speaker_title":"Hon. Ali Sharif","speaker":{"id":2100,"legal_name":"Shariff Athman Ali","slug":"shariff-athman-ali"},"content":" Mhe. Naibu Spika wa Muda, kama nilivyosema, ni masikitiko makubwa kwa sababu nilitarajia Kamati hii ichukue majina ya Wakenya wote waliorudishwa nchini wakiwa wameathirika kwa kudhulumia na kuteswa, halafu waende kule wakafanye uchunguzi kuhusu waathiriwa hao."}