{"id":953071,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/953071/?format=json","text_counter":101,"type":"speech","speaker_name":"Lamu CWR, JP","speaker_title":"Hon. (Ms.) Ruweida Obo","speaker":{"id":786,"legal_name":"Ruweida Mohamed Obo","slug":"ruweida-mohamed-obo"},"content":"Serikali ilisema watu waache kutumia mifuko ya plastiki na hivi sasa hatutumii mifuko hiyo. Mtu akifanya hivyo anafanya kwa siri sana. Inafaa tukijitolea tufanye hivyo pia kuhusu ulanguzi na matumizi ya madawa ya kulevya. Tujisukume zaidi ili tuwachunge watoto wetu. Ahsante."}