{"id":968908,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/968908/?format=json","text_counter":454,"type":"speech","speaker_name":"Mvita, ODM","speaker_title":"Hon. Abdullswamad Nassir","speaker":{"id":2433,"legal_name":"Abdulswamad Sheriff Nassir","slug":"abdulswamad-sheriff-nassir"},"content":"Pili, ni jambo la kusikitisha. Katika ukaguzi, ilitokea wazi hakuna ukaguzi wowote unaoendelea kwa feri hizi. Tulipowauliza wakaguzi kama waliona kuwa milango haifanyi kazi, walisema walikuwa wameona. Hakuna aliyekipofu kujua kwamba milango ya feri haifanyi kazi. Tunaambia KMA kuwa feri zilizobaki zifanyiwe ukaguzi upya, zile cheti wamezitoa za bandia bila kufikiria zirekebishwe. Feri ikiwa haipo sawa, isimamishwe isiendelee kufanya kazi."}