{"id":969809,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/969809/?format=json","text_counter":351,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Faki","speaker_title":"","speaker":{"id":13211,"legal_name":"Mohamed Faki Mwinyihaji","slug":"mohamed-faki-mwinyihaji-2"},"content":"Asante, Bw. Spika. Kulikuwa na ushahidi wa Tume ya Mamlaka ya Sheria; Commission for Administrative Justice. Uamuzi ule ulitolewa kutoka September 2019, ilhali Gavana Waititu hakuchukua fursa yoyote ya kuenda mahakamani kupinga uamuzi ule, wala hakuchukua fursa yoyote ya kuenda katika Tume ile kujitetea ili kuona kwamba jina lake limesafishwa. Kunyamaza wakati Tume kama hii ya kisheria ambayo iko katika Katiba imetoa maamuzi---"}