{"id":969863,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/969863/?format=json","text_counter":405,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Kinyua","speaker_title":"","speaker":{"id":13202,"legal_name":"John Kinyua Nderitu","slug":"john-kinyua-nderitu-2"},"content":"Bw. Spika, kwa hivyo, sisemi ya kwamba Gavana Waititu asisulubiwe. Lakini, kama vile Mahakama Kuu ilisema, mpaka maafikiano na mambo yafuatwe vizuri kabla ya kufanya chochote kwa sababu matokeo yake yatategemea kama tutakuwa tumefuata sheria. Wanasema tumsulubishe lakini, ndugu zangu, ni vizuri kuangalia sheria kwa sababu mambo yote yanapaswa kulingana na mujibu wa sheria zilizowekwa katika nchi yetu ya Kenya."}