{"id":974230,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/974230/?format=json","text_counter":117,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Zawadi","speaker_title":"","speaker":{"id":13176,"legal_name":"Christine Zawadi Gona","slug":"christine-zawadi-gona"},"content":"Bw. Spika, Mhe. Dori alikuwa mwenyekiti wa wabunge wote wa Pwani; wabunge wa Seneti na wale wa Bunge la Kitaifa. Mhe. Dori alipenda sana ushirikiano. Mhe. Dori alipenda tukishirikiana katika mambo ya Bandari ya Mombasa. Alisistiza kwamba bandari ikihamishwa, watu wa Pwani watateseka. Mhe. Dori alikuwa na marafiki kutoka pande zote za Kenya kwani Kwale kunaishi makabila zote. Naamini kwamba kifo cha Mhe. Dori kinahusisha jamii zote za Kenya."}