{"id":983913,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/983913/?format=json","text_counter":278,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Faki","speaker_title":"","speaker":{"id":13211,"legal_name":"Mohamed Faki Mwinyihaji","slug":"mohamed-faki-mwinyihaji-2"},"content":"Bi. Spika wa Muda, ijapokuwa kuna janga la Covid-19, tusifunge macho kwa masuala mengine. Kwa mfano, juzi kwenye barabara ya Mombasa kuelekea Malindi, watu 16 walipoteza maisha yao kutokana na ajali barabarani. Tunaomba the National Transport and Safety Authority (NTSA) iangalie swala hilo. Hatuwezi kuwa tunajitahidi tusipoteze maisha kwa sababu ya Covid-19, ilhali watu wengine wanapoteza maisha katika barabara. Asante."}