{"id":993825,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/993825/?format=json","text_counter":131,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Faki","speaker_title":"","speaker":{"id":13211,"legal_name":"Mohamed Faki Mwinyihaji","slug":"mohamed-faki-mwinyihaji-2"},"content":"Shule nyingi za sehemu za mashambani kama vile Kitui na kwingineko, wanafunzi hawafanyi vizuri katika mitihani yao kwa sababu walimu hawana motisha ya kusomesha. Hii ni kwa sababu hawapati marupurupu yao mapema ili waweze kuwa na hamu ya kufundisha wanafunzi wao."}