{"id":993827,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/993827/?format=json","text_counter":133,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Faki","speaker_title":"","speaker":{"id":13211,"legal_name":"Mohamed Faki Mwinyihaji","slug":"mohamed-faki-mwinyihaji-2"},"content":"Iwapo suala hilo halitachunguzwa vizuri ina maana kwamba nchi nzima wanafunzi watapata hasara kwa sababu walimu wanaowasomesha hawana motisha. Naomba kamati ambayo itashughulikia suala hili iingilie ndani na isisimame Kitui pekee, bali Kenya nzima ili liweze kutatuliwa mara moja."}