GET /api/v0.1/hansard/entries/111005/?format=api
HTTP 200 OK
Allow: GET, PUT, PATCH, DELETE, HEAD, OPTIONS
Content-Type: application/json
Vary: Accept
{
"id": 111005,
"url": "https://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/111005/?format=api",
"text_counter": 248,
"type": "speech",
"speaker_name": "Mr. Mungatana",
"speaker_title": "",
"speaker": {
"id": 185,
"legal_name": "Danson Buya Mungatana",
"slug": "danson-mungatana"
},
"content": "Ukiniuliza mimi kama Katiba hii imeenda mbele katika demokrasia au la, nina jibu langu. Lakini wewe mwananchi na wenzangu pia mna majibu yenu. Hakuna mtu atakayekujibu zaidi ya hapo. Ukiangalia siku ya Jumanne, na siku zote tunapokuja hapa kwa vikao vya Bunge, hawako. Kazi zao za maeneo yao ya bunge zinachukua nafasi ya mbele kwa sababu walikuwa wabunge kwanza kisha wakawa mawaziri. Sasa tumepitisha katika Katiba hii ya kwamba wewe ukiwa waziri, fanya kazi yako ya uwaziri. Wewe ukiwa mbunge ama seneta, fanya kazi yako ya ubunge ama useneta. Ikiwa unafanya kazi yako ya kupitisha sheria, fanya kazi yako ya kupitisha sheria. Tumekuwa na sakata hapa juzi kuhusu mawaziri na makatibu wa kudumu katika wizara. Wakati ambapo ilikuja ya watu kufutwa kazi, makatibu wa kudumu watano walifutwa kazi kwa wakati moja. Hakuna mtu aliyetoa tone moja la jicho angalau kusema pole ama chozi moja; hata chozi la mamba la uongo. Hakuna hata mtu aliyesema. Lakini ilipokuja wakati wa kufuta mawaziri kazi; hawakufutwa kazi. Waliambiwa tu: Ondoka tu, tufanye uchuguguzi. Tunataka mfumo ambao utasema: âWewe utakuwa chini ya jicho la Bunge. Wewe ni waziri lakini uko chini ya jicho la Bunge. Ukifanya makosa, utafukuzwa kama vile makatibu wa kudumu walivyofanywa. Ukiniambia je hii Katiba ambayo niko nayo ambayo ilimfanya waziri awe na nguvu kupita kiasi, na hii ambayo tunaitaka sasa, nzuri ni ipi? Jibu ni lako. Bunge letu lina nguvu kusema ukweli. Lakini Bunge letu la sasa halina nguvu ya kumfukuza Rais. Kwa sababu ukimfukuza Rais, Bunge letu pia linakufa. Hii inamaanisha kwamba tunajinyonga sote. Kutumia kipengele hicho, Rais aliweza kufanya mambo mengi kupitia Katiba hii ya zamani. Katika Katiba hii mpya, Rais akifanya mambo mabaya, Bunge limepewa mamlaka, tukipata thuluthi tatu hapa Bunge na likienda kwa bunge la senate, Rais anaenda kwao. Tena sio kuwa eti nchi itakuwa katika taabu; hakuna. Kuna Makamu wa Rais ambaye amechaguliwa na wananchi. Zamani, ilikuwa Rais ako na nguvu mpaka anasema kwani nikiwapatia huyu Makamu wa Rais ndiyo mtaongezea ugali katika sufuria zenu? âHaya chukueni Makamu wa Rais.â Makamu wa Rais alikuwa anachaguliwa kwa bara bara. Jambo hilo halitatendeka tena. Sitaki mtoto wangu, mjukuu wangu wala kitukuu changu kiishi chini ya Katiba hii ya zamani. Bw. Naibu Spika wa Muda, wakati huu tuko na Makamu wa Rais ambaye tulimchagua. Kwa hivyo, Rais akitimuliwa kutoka mamlakani kwa sababu ya kuiba au kufanya uhaini, basi Makamu wa Rais atachukua mamlaka na nchi yetu itaendelea bila shida yoyote. Lakini kama hatuna Makamu wa Rais, basi Spika wa Bunge atachukua mamlaka kuambatana na Katiba hii mpya. Ukiniuliza kati ya Katiba ya sasa na hii mpya, ni ipi nzuri, jibu nitakuwachia wewe mwenyewe. Ukiangalia kipengele juu ya Parliamentary Service Commission (PSC), utaona kimewekwa vizuri zaidi chini ya Katiba hii mpya. Ukiangalia jinsi tunavyopitisha sheria hapa Bungeni au the legislative programming and making laws in this country, utaona kuwa imewekwa vizuri sana katika Katiba hii mpya kushinda ilivyo katika Katiba ya sasa. Ukiangalia kipengele juu ya uteuzi wa majaji au mahakimu wa mahakama zetu umeelezwa vizuri katika Katiba hii kuliko ya zamani. Uteuzi wa majaji chini ya Katiba ya sasa, haufanywi kwa njia ya haki. Utaona ni wale watu ambao wanajulikana kwa wakuu wa nchi; Rais, Waziri anayehusika au wakuu wa Civil Service, wanachaguliwa na kuapishwa hata kama rekodi zao si nzuri. Wakati mwingine, mtu anayechaguliwa kama jaji anajua kuwa ana dosari fulani na hata Waziri anayehusika anajua kuna shida, lakini"
}