GET /api/v0.1/hansard/entries/590680/?format=api
HTTP 200 OK
Allow: GET, PUT, PATCH, DELETE, HEAD, OPTIONS
Content-Type: application/json
Vary: Accept
{
"id": 590680,
"url": "https://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/590680/?format=api",
"text_counter": 343,
"type": "speech",
"speaker_name": "Sen. Muthama",
"speaker_title": "",
"speaker": {
"id": 96,
"legal_name": "Johnson Nduya Muthama",
"slug": "johnson-muthama"
},
"content": "Bw. Spika wa muda, nakubaliana nawe lakini nilikuwa tu natoa uwazi kwamba kutokana na Hotuba ya Rais Kikwete, alitaka tuungane kama Watanzania. Kwa hivyo, kama tutakubalike na mataifa mengine, ni lazima tutembee katika misingi ya usafi na kufanya mambo yanayolingana na uongozi unaotakiwa. Taifa letu la Kenya, tukiungana na wenzetu na kufanya kazi nao, ni lazima tuhakikishe tunaheshimiwa kule nje. Ndugu yangu, Sen. G.G. Kariuki, amesema jambo la maana sana ya kwamba, si kwamba rais akiwa wa kabila fulani, kabila hilo litakuwa salama. Ni lazima Wakenya walindwe na sheria zilizoko. Leo hii, tumepoteza mwelekeo. Nimewasihi ndugu zangu wa mrengo wa Jubilee waepukane na uvumi wanaoueneza kila pembe ya nchi hii wakidai; “Raila kafanya haya na huyu kafanya haya”. Wao wanafikiri watammaliza mtu fulani kisiasa. Chuki wanayoiendesha nchini itamaliza kesho yetu. Mimi nlikuwa kiranja wa Bunge la Kumi. Ninafahamu wazi kwamba Mhe. Raila hangeweza kumtia Mhe. Ruto katika mashaka. Mhe. Ruto alikuwa rafiki wake wa karibu sana na alikuwa anamsaidia kuongoza chama. Hawa viongozi wa Jubilee wanadhani Wakenya watakuwa vipofu tu mara moja, na kusahau yaliyotokea kwa kusema Mhe. Raila Amolo Odinga alihusika kumsingizia Mhe. Naibu Rais. Lazima tuongee ukweli. Watanzania hawawezi kuongea kama sisi. Shida ya leo ni watu wawili katika taifa letu---"
}