GET /api/v0.1/hansard/entries/277828/?format=api
HTTP 200 OK
Allow: GET, PUT, PATCH, DELETE, HEAD, OPTIONS
Content-Type: application/json
Vary: Accept
{
"id": 277828,
"url": "https://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/277828/?format=api",
"text_counter": 299,
"type": "speech",
"speaker_name": "Mr. Joho",
"speaker_title": "The Assistant Minister for Transport",
"speaker": {
"id": 30,
"legal_name": "Hassan Ali Joho",
"slug": "hassan-joho"
},
"content": " Bi. Naibu Spika wa Muda, naona kuwa ndugu yangu hajajua jambo la nidhambu ni nini. Nimesema hivyo kwa sababu sina raha kuona mtu anasema ati sisi ni GEMA; sisi ni KAMATUSA; tunataka tusikie kuwa sisi ni Wakenya. Ninasema hivi, hata kwa wale ndugu zangu walioko Mombasa; nawaambia wasiseme kuwa Pwani si Kenya. Ningefurahi hata viongozi wa kutoka maeneo ya GEMA, KAMATUSA na kadhalika wakisema kwanza wao ni Wakenya. Kwa hivyo hiyo isikutishe; pengine Kiswahili chakuchanganya. Baadaye tukitoka pale nje, nitakuambia kwa Kimombo ili uelewe vizuri."
}