GET /api/v0.1/hansard/entries/7643/?format=api
HTTP 200 OK
Allow: GET, PUT, PATCH, DELETE, HEAD, OPTIONS
Content-Type: application/json
Vary: Accept

{
    "id": 7643,
    "url": "https://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/7643/?format=api",
    "text_counter": 306,
    "type": "speech",
    "speaker_name": "Mr. Ethuro",
    "speaker_title": "",
    "speaker": {
        "id": 158,
        "legal_name": "Ekwee David Ethuro",
        "slug": "ekwee-ethuro"
    },
    "content": "Bw. Naibu Spika wa Muda, ningependa kumshukuru Waziri kwa Kiswahili sanifu. Waziri amesema kuwa barabara kutoka Kachibora hadi Sibanga inaelekea Kitale. Ningependa kumkumbusha Waziri kwamba, - inafaa ajue - barabara kutoka Kachibora mpaka Sibanga inapitia Makutano, Kapenguria mpaka Lodwar. Kwa vile amesema atatengeneza barabara hizo zote, je, atarekebisha lini barabara ya Sibanga- Makutano-Kapenguria-Lodwar? Ametenga pesa ngapi za kurekebisha barabara hii ili nami nimwalike Rais aje aifungue barabara hiyo?"
}