HTTP 200 OK
Allow: GET, POST, HEAD, OPTIONS
Content-Type: application/json
Vary: Accept
{
"count": 1608389,
"next": "https://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/?format=api&page=154101",
"previous": "https://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/?format=api&page=154099",
"results": [
{
"id": 1559192,
"url": "https://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1559192/?format=api",
"text_counter": 183,
"type": "speech",
"speaker_name": "Hon. Speaker",
"speaker_title": "",
"speaker": null,
"content": "Zungumza kwa Kiswahili ili wageni wako wakuelewe."
},
{
"id": 1559193,
"url": "https://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1559193/?format=api",
"text_counter": 184,
"type": "speech",
"speaker_name": "Taveta, WDM",
"speaker_title": "Hon. John Bwire",
"speaker": null,
"content": " Ahsante, Mhe. Spika. Kifungu cha 56 cha Katiba ya Kenya kinatoa mwelekeo kwamba Serikali itafanya mipango ya kutambua jamii ndogo nchini Kenya. Hiyo mipango itaongeza mambo ya utawala, kazi na kutambua mila na desturi zao. Ninakumbuka ulipokuja Eneo Bunge langu mwaka wa 2023, wazee walio mbele yako leo walikueleza kwamba wangetamani sana watambulike kama moja ya makabila ya Kenya. Ninakumbuka hiyo siku uliwaeleza kwamba kuchelewa kutambulishwa kwao ni kinyume cha Katiba. Na kwamba, kama jamii zingine kama vile jamii ya Wasomali kwenye mpaka wa Kenya na Somalia, Waluo katika mpaka wa Kenya na Tanzania, na Wakuria katika mpaka wa Kenya na Tanzania, Wapare walioko kwenye mpaka wa Kenya na Tanzania kule Taveta, watambulike. Leo hii, ninatoa shukrani kwa niaba ya kamati ya wazee wa Wapare wanaoishi sehemu zingine za Kenya na Eneo Bunge la Taveta. Ninakushukuru Mhe. Spika na Bunge hili la Kitaifa kwa kuwapatia nafasi ya kuleta malalamishi yao Bungeni. Wamesikilizwa na wamepewa hakikisho kwamba maombi yao yataangaliwa. Ningependa kusema jambo moja tu kabla niketi. Mwaka wa 2022, mmoja wa jamii hii, alipendekezwa kuwa mwakilishi kata maalum kwa Chama cha Wiper ilhali nafasi ilichukuliwa. Baada ya kuenda kortini, korti ikasema kuwa kwa sababu Wapare wanatambulika kama wasio na nchi, waliwekwa kimakosa katika orodha ya jamii walio wachache nchini ilhali hali sio vile. Kwa hivyo, hatua hii ambayo imechukuliwa na Bunge la kitaifa leo ni ya kipekee sana. Ninachukua nafasi hii kumshukuru Mhe. Spika na Wajumbe wenzangu kwa kuwapatia Wapare nafasi hata ya kufika Bunge leo. Wengine wao wameniambia hawajawahi kutambulika katika Bunge la Kitaifa. Mhe. Spika, asante kwa kuwatambua leo na Mwenyezi Mungu aendelee kukubariki. Asante Sana."
},
{
"id": 1559194,
"url": "https://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1559194/?format=api",
"text_counter": 185,
"type": "speech",
"speaker_name": "Hon. Speaker",
"speaker_title": "",
"speaker": null,
"content": "Ahsante Mhe. Bwire. Mhe. wa Kisauni."
},
{
"id": 1559195,
"url": "https://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1559195/?format=api",
"text_counter": 186,
"type": "speech",
"speaker_name": "Kisauni, ODM",
"speaker_title": "Hon. Rashid Bedzimba",
"speaker": {
"id": 13383,
"legal_name": "Ali Menza Mbogo",
"slug": "ali-menza-mbogo"
},
"content": " Asante sana, Mhe. Spika kwa kunipatia fursa hii ili nitilie nguvu swala la ndugu yetu, Mhe. Bwire. The electronic version of the Official Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Hansard Editor."
},
{
"id": 1559196,
"url": "https://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1559196/?format=api",
"text_counter": 187,
"type": "speech",
"speaker_name": "Kisauni, ODM",
"speaker_title": "Hon. Rashid Bedzimba",
"speaker": {
"id": 13383,
"legal_name": "Ali Menza Mbogo",
"slug": "ali-menza-mbogo"
},
"content": "Pia nami, ninawapongeza wazee Wapare waliopata nafasi ya kufika Bunge hili. Pia, natilia mkazo na nguvu kwamba watambuliwe. Kule mashinani, wanapata shida kubwa kuanzia hao wazee mpaka watoto wao. Hata katika shule ya msingi siku hizi, lazima uwe na stakabadhi ya kuzaliwa ndio usajiliwe kama mwanafunzi. Inakuwa ni vigumu kwa watoto na wajukuu wao. Hii ni jamii ya Kenya. Hawaishi mahali pengine. Wanaweza kuwa upande wa Tanzania, lakini Wapare wengine ni Wakenya, ambao tuko nao mpaka Eneo Bunge ya Kisauni na sehemu zingine. Kwa hivyo, nasimama hapa kutilia nguvu watambuliwe kama Wakenya kwa haraka kama jamii ya Pemba. Wale waliobaki waendelee kutambuliwa, bora wako Kenya, ili kusudi waweze kuajiriwa na kufanya mambo yote raia wanafanya. Mhe. Spika, nimesimama kuunga mkono na kusisitiza hili jambo lichukuliwe kwa haraka, ili wasipate tabu na adhabu wanazoendelea kupata."
},
{
"id": 1559197,
"url": "https://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1559197/?format=api",
"text_counter": 188,
"type": "speech",
"speaker_name": "Kisauni, ODM",
"speaker_title": "Hon. Rashid Bedzimba",
"speaker": {
"id": 13383,
"legal_name": "Ali Menza Mbogo",
"slug": "ali-menza-mbogo"
},
"content": "Asante sana."
},
{
"id": 1559198,
"url": "https://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1559198/?format=api",
"text_counter": 189,
"type": "speech",
"speaker_name": "Hon. Speaker",
"speaker_title": "",
"speaker": null,
"content": "Hon. Owen Baya."
},
{
"id": 1559199,
"url": "https://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1559199/?format=api",
"text_counter": 190,
"type": "speech",
"speaker_name": "Hon. Members",
"speaker_title": "",
"speaker": null,
"content": "Ongea kwa Kiswahili."
},
{
"id": 1559200,
"url": "https://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1559200/?format=api",
"text_counter": 191,
"type": "speech",
"speaker_name": "Kilifi North, UDA",
"speaker_title": "Hon. Owen Baya",
"speaker": null,
"content": " Hon. Speaker, allow me to express myself best in English."
},
{
"id": 1559201,
"url": "https://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1559201/?format=api",
"text_counter": 192,
"type": "scene",
"speaker_name": "",
"speaker_title": "",
"speaker": null,
"content": "(Loud consultation)"
}
]
}