Ali Menza Mbogo

Parties & Coalitions

All parliamentary appearances

Entries 1 to 10 of 295.

  • 23 Apr 2025 in National Assembly: Asante sana, Mhe. Spika kwa kunipatia fursa hii ili nitilie nguvu swala la ndugu yetu, Mhe. Bwire. The electronic version of the Official Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Hansard Editor. view
  • 23 Apr 2025 in National Assembly: Pia nami, ninawapongeza wazee Wapare waliopata nafasi ya kufika Bunge hili. Pia, natilia mkazo na nguvu kwamba watambuliwe. Kule mashinani, wanapata shida kubwa kuanzia hao wazee mpaka watoto wao. Hata katika shule ya msingi siku hizi, lazima uwe na stakabadhi ya kuzaliwa ndio usajiliwe kama mwanafunzi. Inakuwa ni vigumu kwa watoto na wajukuu wao. Hii ni jamii ya Kenya. Hawaishi mahali pengine. Wanaweza kuwa upande wa Tanzania, lakini Wapare wengine ni Wakenya, ambao tuko nao mpaka Eneo Bunge ya Kisauni na sehemu zingine. Kwa hivyo, nasimama hapa kutilia nguvu watambuliwe kama Wakenya kwa haraka kama jamii ya Pemba. Wale waliobaki ... view
  • 23 Apr 2025 in National Assembly: Asante sana. view
  • 4 Mar 2025 in National Assembly: Ahsante sana Mhe. Spika wa Muda. Nami pia nasimama miongoni mwa wanaounga mkono maslaha ya maafisa wa usalama wa ndani. Wanafanya jukumu kubwa sana. Huu usalama wote ulio katika taifa hili ni jukumu lao. Ingawa wako wanaofanya matatizo na makosa, siyo wote. Maslaha yao yaangaliwe zaidi. Nimefanya kazi ya polisi kwa miaka tisa na nilipata shida kubwa mno. Nimehangaishwa Kenya nzima. Natolewa stesheni hii baada ya miezi sita, napelekwa nyingine kwa miezi sita. Tulikuwa tunatembea na sanduku la chakula na safari bed. Tungeingia katika hali nyingine ambapo hema zingekuwa ni matope matupu, ilhali hapo ndipo tunapikia. Nimefanya katika Kikosi cha view
  • 4 Mar 2025 in National Assembly: na najua shida wanazozipitia. Kwa hivyo, ni vyema tuangalie maslaha yao. The electronic version of the Official Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Hansard Editor. view
  • 4 Mar 2025 in National Assembly: Ni lazima wawekewe bima. Wakati mwingine, wao hupata ulemavu wakienda kazini na kurudi manyumbani mwao kuteseka na familia zao. Watoto wao hawasomi vizuri kwa kuwa wanahamishwa hapa na pale. Inafaa wawe wanajengewa chuo cha maafisa wa polisi na watoto wao waishi pale kwa uzuri, ili maafisa wafanye kazi kwa utulivu. Hivi sasa, wanaishi katika hali ngumu sana. Wanalala katika sehemu iliyogawanywa na nguo ya aina ya leso tu! Mmoja yuko upande huu na mwingine upande ule. Wakati mwingine, mmoja anapewa zamu ya usiku ilhali afisa mwenzake anabaki pale nyumbani. Saa nyingine, wake wa wengine wamehama na wako nao pale. Utaenda ... view
  • 18 Feb 2025 in National Assembly: Ahsante sana, Mhe. Spika. Nasimama kwa niaba ya Eneo Bunge la Kisauni kusema pole kwa ndugu, jamaa na marafiki wa Eneo Bunge la Malava kwa kifo cha Mhe. Injendi ambaye aliishi na watu vizuri. Anachohitaji sasa ni maombi. Tumuombee Mungu amsamehe dhambi zake na amuweke mahala pema peponi. Kifo chake kinatukumbusha kuwa duniani, tunapitia tu. Unalohitajika kufanya duniani ni mambo mema. Hayo ndiyo yatakayokusaidia mbele. Kifo hakijali ikiwa wewe ni mtu mzima, mtoto, wala cheo ulichonacho. Hakuna mtu aliye na uhakika wa kuishi dakika mbili The electronic version of the Official Hansard Report is for information purposesonly. A certified version ... view
  • 18 Feb 2025 in National Assembly: kutoka sasa. Wale walio hai wajue kuwa kuna safari ambayo wanaelekea na watende mema. Sisi tuliopewa jukumu la uongozi tuwasaidie waliotuchagua. Ahsante, Mhe. Spika. view
  • 25 Nov 2024 in National Assembly: Ahsante sana, Mhe. Spika wa Muda, kwa kunipa fursa hii nami niweze kupenyeza sauti yangu kwa kuichangia Hotuba ya Rais aliyokuja kuzungumza hapa, kwa taifa. view
  • 25 Nov 2024 in National Assembly: Kwanza, nizungumzie swala la Adani. Kwa kuivunjilia mbali kandarasi ya Adani, Mhe. Rais amefurahisha Wakenya wengi kwa sababu ni jambo ambalo lilikua limeleta utata mkubwa. Wafanyikazi wote walikuwa na wasiwasi kwamba badala ya kulipwa kwa mwezi, watabadilishwa kuwa na mikataba. Ni jambo la utata mkubwa kuona rasilimali yetu tunayoitegemea, mtu akikuja kuisimamia kwa miaka 30. Kwa hivyo, ilikua ni wasiwasi mkubwa. Alipoifutilia mbali, amefanya jambo nzuri. Amesikiliza wananchi, na kiongozi yeyote ni yule anayesikiliza wananchi. Kwa hivyo, hilo nampongeza Mhe. Rais. view

Comments

(For newest comments first please choose 'Newest' from the 'Discussion' tab below.)
comments powered by Disqus