Ali Menza Mbogo

Parties & Coalitions

All parliamentary appearances

Entries 1 to 10 of 292.

  • 4 Mar 2025 in National Assembly: Ahsante sana Mhe. Spika wa Muda. Nami pia nasimama miongoni mwa wanaounga mkono maslaha ya maafisa wa usalama wa ndani. Wanafanya jukumu kubwa sana. Huu usalama wote ulio katika taifa hili ni jukumu lao. Ingawa wako wanaofanya matatizo na makosa, siyo wote. Maslaha yao yaangaliwe zaidi. Nimefanya kazi ya polisi kwa miaka tisa na nilipata shida kubwa mno. Nimehangaishwa Kenya nzima. Natolewa stesheni hii baada ya miezi sita, napelekwa nyingine kwa miezi sita. Tulikuwa tunatembea na sanduku la chakula na safari bed. Tungeingia katika hali nyingine ambapo hema zingekuwa ni matope matupu, ilhali hapo ndipo tunapikia. Nimefanya katika Kikosi cha view
  • 4 Mar 2025 in National Assembly: na najua shida wanazozipitia. Kwa hivyo, ni vyema tuangalie maslaha yao. The electronic version of the Official Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Hansard Editor. view
  • 4 Mar 2025 in National Assembly: Ni lazima wawekewe bima. Wakati mwingine, wao hupata ulemavu wakienda kazini na kurudi manyumbani mwao kuteseka na familia zao. Watoto wao hawasomi vizuri kwa kuwa wanahamishwa hapa na pale. Inafaa wawe wanajengewa chuo cha maafisa wa polisi na watoto wao waishi pale kwa uzuri, ili maafisa wafanye kazi kwa utulivu. Hivi sasa, wanaishi katika hali ngumu sana. Wanalala katika sehemu iliyogawanywa na nguo ya aina ya leso tu! Mmoja yuko upande huu na mwingine upande ule. Wakati mwingine, mmoja anapewa zamu ya usiku ilhali afisa mwenzake anabaki pale nyumbani. Saa nyingine, wake wa wengine wamehama na wako nao pale. Utaenda ... view
  • 18 Feb 2025 in National Assembly: Ahsante sana, Mhe. Spika. Nasimama kwa niaba ya Eneo Bunge la Kisauni kusema pole kwa ndugu, jamaa na marafiki wa Eneo Bunge la Malava kwa kifo cha Mhe. Injendi ambaye aliishi na watu vizuri. Anachohitaji sasa ni maombi. Tumuombee Mungu amsamehe dhambi zake na amuweke mahala pema peponi. Kifo chake kinatukumbusha kuwa duniani, tunapitia tu. Unalohitajika kufanya duniani ni mambo mema. Hayo ndiyo yatakayokusaidia mbele. Kifo hakijali ikiwa wewe ni mtu mzima, mtoto, wala cheo ulichonacho. Hakuna mtu aliye na uhakika wa kuishi dakika mbili The electronic version of the Official Hansard Report is for information purposesonly. A certified version ... view
  • 18 Feb 2025 in National Assembly: kutoka sasa. Wale walio hai wajue kuwa kuna safari ambayo wanaelekea na watende mema. Sisi tuliopewa jukumu la uongozi tuwasaidie waliotuchagua. Ahsante, Mhe. Spika. view
  • 25 Nov 2024 in National Assembly: Ahsante sana, Mhe. Spika wa Muda, kwa kunipa fursa hii nami niweze kupenyeza sauti yangu kwa kuichangia Hotuba ya Rais aliyokuja kuzungumza hapa, kwa taifa. view
  • 25 Nov 2024 in National Assembly: Kwanza, nizungumzie swala la Adani. Kwa kuivunjilia mbali kandarasi ya Adani, Mhe. Rais amefurahisha Wakenya wengi kwa sababu ni jambo ambalo lilikua limeleta utata mkubwa. Wafanyikazi wote walikuwa na wasiwasi kwamba badala ya kulipwa kwa mwezi, watabadilishwa kuwa na mikataba. Ni jambo la utata mkubwa kuona rasilimali yetu tunayoitegemea, mtu akikuja kuisimamia kwa miaka 30. Kwa hivyo, ilikua ni wasiwasi mkubwa. Alipoifutilia mbali, amefanya jambo nzuri. Amesikiliza wananchi, na kiongozi yeyote ni yule anayesikiliza wananchi. Kwa hivyo, hilo nampongeza Mhe. Rais. view
  • 25 Nov 2024 in National Assembly: Nikija katika upande wa shilingi kuwa na nguvu, ni kweli, shilingi yetu ilikuwa imekosa thamani kubwa. Hata ilikuwa ukienda kwa nchi jirani kubadilisha pesa yetu ya Kenya wanaikataa. Wanasema pesa ya Kenya haieleweki kwa maana leo iko hivi, kesho iko chini zaidi. Lakini imeimarishwa na mpaka sasa pesa yetu inaheshimika. Kushuka kwa dola, sisi tunategemea kwamba taifa litaimarika wakati pesa za kigeni na hali ya uchumi kama mafuta yataweza kushuka bei. Isipande kwa sababu dola imeanguka. Kwa hivyo, wananchi wanategemea wakati dola imeendelea vizuri na pesa zitashuka ili kusudi mwananchi aweze kujikimu ama gharama za maisha zisiweze kupanda juu. view
  • 25 Nov 2024 in National Assembly: Tuje katika upande wa SHA. Mimi mwenyewe nimeweza kushuhudia wagonjwa wa moyo katika Hospitali ya Rufaa ya Mombasa, yaani Coast General Hospital . Kuna mgonjwa ambaye alienda kuwekewa pacemaker au kifaa ambacho kinaweza kufanya moyo wake upige kwa usawa, bill yake ikaja Ksh1.3 milioni. Na nikashangaa kuona SHA imemlipia Ksh1.1 milioni papo hapo. Kwa hivyo, nimeona ni jambo ambalo kama watalitilia bidii; kama hawatabadilika, hii SHA itasaidia sana mwananchi wa kawaida. Na vile vile, ukiangalia SHA katika levels 2, 3, 4 hospitals, ukipiga tu kwenye simu yako *147# ili kujisajili, wewe unatibiwa bila malipo. Ikiwa itaendelezwa vile inavyoendelea sasa, itawasaidia ... view
  • 25 Nov 2024 in National Assembly: Hivi sasa, SHA kwa mwezi ni shilingi Ksh300, NHIF ilikuwa Ksh500. Kwa hivyo SHA kwa mwaka ni Ksh3,600. Nina imani kwamba ikiwa watajipanga vizuri, itakuwa jambo la busara kwa sababu matibabu ni ghali sana na mwananchi wa kawaida hawezi kulipa. Katika NHIF, kulikuwa na uzito mmoja. Wakati unaambiwa unangoja approval, unaweza kungoja masaa matatu au matano kabla kupewa hiyo ruhusa ya kupewa dawa ama kuruhusiwa kwenda nyumbani. Lakini SHA kwa sasa ni kwamba ukingoja approval, hauchukui muda. Kwa hivyo, ikiwa wataendelea namna hii, basi itasaidia wananchi sana. Juzi tu nimetembelea hiyo hospitali na SHA wamelipa kufikia sasa Ksh21.9 milioni kwa ... view

Comments

(For newest comments first please choose 'Newest' from the 'Discussion' tab below.)
comments powered by Disqus