HTTP 200 OK
Allow: GET, POST, HEAD, OPTIONS
Content-Type: application/json
Vary: Accept
{
"count": 1608389,
"next": "https://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/?format=api&page=154275",
"previous": "https://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/?format=api&page=154273",
"results": [
{
"id": 1560932,
"url": "https://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1560932/?format=api",
"text_counter": 184,
"type": "speech",
"speaker_name": "Suba North, ODM",
"speaker_title": "Hon. Millie Odhiambo-Mabona",
"speaker": null,
"content": " Thank you, Hon. Temporary Speaker. We indeed have a broad-based government arrangement. I speak cautiously as a lawyer. Within the broad-based government arrangement, I undertake that this matter shall be responded to within two weeks after the House resumes from recess due to its urgency."
},
{
"id": 1560933,
"url": "https://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1560933/?format=api",
"text_counter": 185,
"type": "speech",
"speaker_name": "Hon. Farah Maalim",
"speaker_title": "The Temporary Speaker",
"speaker": {
"id": 16,
"legal_name": "Farah Maalim Mohamed",
"slug": "farah-maalim"
},
"content": " Very well, that is acceptable. The next request for Statement will be from the Member for Msambweni, Hon. Faisal Bader."
},
{
"id": 1560934,
"url": "https://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1560934/?format=api",
"text_counter": 186,
"type": "heading",
"speaker_name": "",
"speaker_title": "",
"speaker": null,
"content": "UNYAKUZI WA ARDHI YA MSIKITI WA KONGO KATIKA ENEOBUNGE LA MSAMBWENI"
},
{
"id": 1560935,
"url": "https://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1560935/?format=api",
"text_counter": 187,
"type": "speech",
"speaker_name": "Msambweni, UDA",
"speaker_title": "Mhe. Feisal Bader",
"speaker": null,
"content": " Ahsante, Mhe. Spika wa Muda. Kwa mujibu wa Kanuni ya Kudumu ya 44(2)(c), naomba Kauli kutoka kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Ardhi kuhusu unyakuzi wa ardhi ya umma ya Msikiti wa Kongo katika Eneobunge la Msambweni. Mheshimiwa Spika, Msikiti wa Kongo una dhima ya kihistoria na kidini, kwa kuwa ulijengwa katika Karne ya 14 na Waajemi (Persians). Msikiti huu ulitambuliwa kwa mara ya kwanza kama kumbukumbu la kitaifa na Serikali ya mkoloni mnamo mwezi Juni mwaka wa 1927. Baada ya Kenya kupata uhuru, Msikiti wa Kongo, pamoja na ardhi inayouzunguka, ulitangazwa rasmi kuwa kumbukumbu la kitaifa lililolindwa chini ya sheria. Hata hivyo, mnamo mwaka wa 1986, inadaiwa kwamba watu fulani walishirikiana na maafisa waandamizi wa Serikali kutekeleza njama ya kumilikishwa ardhi hiyo kwa Rais wa wakati huo, hayati Daniel Toroitich Arap Moi, kwa njia ya udanganyifu na isiyo halali. Mnamo mwaka wa 2009, akiwa amestaafu, hayati Rais Moi alifahamishwa kuhusu umilikishaji huo usiyo halali na kwa hiari yake, alirejesha hati miliki ya ardhi hiyo kwa msajili wa hati. Hatua hii ilipelekea kubatilishwa kwa hati miliki hiyo na kurejesha hali ya umiliki wa ardhi hiyo kuwa ya umma, kama ilivyotambuliwa tangu mwaka wa 1927. Mhe. Spika wa Muda, kutokana na hatua hizo, Serikali ilitenga ardhi hiyo kwa manufaa ya jamii ya Waislamu wanaoswali katika Msikiti wa Kongo na kutoa hati mbili: Hati Nambari 55034 kwa Msikiti wa Kongo na Hati Nambari 55035 kwa Kituo cha Kiislamu cha Kwale. Serikali iliteua Katibu Mtendaji katika Wizara ya Hazina ya Taifa kuwa mdhamini wa hati miliki ya ardhi hiyo. Mnamo mwaka wa 2012, aliyekuwa Waziri Mkuu wakati huo, Mhe. Raila Odinga, maarufu Baba, alizikabidhi hati miliki hizo kwa jamii-nufaika. Mnamo mwezi wa Machi 2025, jamii hiyo ilishangaa kugundua kuwa kipande hicho cha ardhi kilikuwa kimetangazwa kuuzwa kwa bei ya shilingi bilioni moja, milioni mia nne arobaini na tano (Ksh1.445 bilioni). Watu wanaodai kumiliki ardhi hiyo ni Bwana Mohammed Hamisi Mwachumba na Bwana Ali Mwadarashi Mwagariche. Wanadai kuwa walipata hati miliki ya ardhi hiyo tarehe 17 Februari 2025. Jambo ambalo linastaajabisha ni kuwa The electronic version of the Official Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Hansard Editor."
},
{
"id": 1560936,
"url": "https://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1560936/?format=api",
"text_counter": 188,
"type": "speech",
"speaker_name": "Msambweni, UDA",
"speaker_title": "Mhe. Feisal Bader",
"speaker": null,
"content": "inafahamika kwamba ardhi hiyo imekuwa ya umma tangu mwaka wa 1927 na kudumishwa baada ya Kenya kuwa nchi huru. Mhe. Spika wa Muda, ni kutokana na hali hii ndipo ninaomba kauli kutoka kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Kiidara ya Ardhi kuhusu masuala yafuatayo: 1. Maelezo kuhusu namna ambavyo ardhi ya Msikiti wa Kongo, inayojulikana kuwa ardhi ya umma na iliyotangazwa kama eneo la kumbukumbu la kitaifa lililolindwa, ilisajiliwa kwa umiliki wa kibinafsi. 2. Hatua zinazochukuliwa na Wizara ya Ardhi pamoja na Tume ya Kitaifa ya Ardhi kukabiliana na unyakuzi huu wa ardhi ya Msikiti wa Kongo. 3. Mikakati iliyowekwa kulinda eneo hilo kama kumbukumbu la kitaifa linalolindwa. 4. Maelezo ya kina kuhusu jinsi Wizara pamoja na Tume ya Kitaifa ya Ardhi zinavyokusudia kuwezesha kurejeshwa kwa ardhi hiyo kwa wamiliki halali ambao ni jamii ya Waislamu wa Msikiti wa Kongo. Asante, Mhe. Spika wa Muda."
},
{
"id": 1560937,
"url": "https://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1560937/?format=api",
"text_counter": 189,
"type": "speech",
"speaker_name": "Hon. Farah Maalim",
"speaker_title": "The Temporary Speaker",
"speaker": {
"id": 16,
"legal_name": "Farah Maalim Mohamed",
"slug": "farah-maalim"
},
"content": " Kuna Mhe. yeyote angependa kuchangia Kauli hii? Dada yetu kutoka Kwale, Mhe. Masito."
},
{
"id": 1560938,
"url": "https://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1560938/?format=api",
"text_counter": 190,
"type": "speech",
"speaker_name": "Kwale County, ODM",
"speaker_title": "Hon. Fatuma Masito",
"speaker": null,
"content": " Asante sana, Mhe. Spika wa Muda, kwa kunipa fursa hii. Nataka ibaki katika kumbukumbu za Bunge hili kwamba naunga mkono Kauli iliyoletwa na Mbunge wa Msambweni. Yeye ametoka katika eneo bunge ambayo mimi pia ninamiliki. Sisi, kama watu wa Kwale, tulitamaushwa pakubwa na jambo hili. Mimi naunga mkono Kauli hii. Hii ni kwa sababu mimi ni mtoto wa Kiislamu na ninaelewa historia kamili kama vile Mhe. Feisal alivyo izungumzia. Ardhi ya Msikiti wa Kongo ni pahali patakatifu. Ni jambo la kushangaza vile wezi na walaghai walikuja na kusema ardhi ile wao ndio wamiliki. Historia inajieleza vizuri sana kwamba ardhi ile ni ya msikiti. Ilipatikana kwa njia gani? Mhe. Feisal ameeleza historia. Haiwezekani kuwa mtu ametokezea hivi majuzi na anasema anataka kumiliki ardhi ile ya kihistoria. Ardhi ya Kongo haiuziki na haiwezi kuuzwa. Nina laani vikali jambo hili. Pia, naongezea Kamati ya Kiidara ya Ardhi ya Bunge hili iweze kuingilia kati. Hii ni kwa sababu historia inajieleza vizuri sana. Wacha nikome hapo. Asante sana."
},
{
"id": 1560939,
"url": "https://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1560939/?format=api",
"text_counter": 191,
"type": "speech",
"speaker_name": "Hon. Farah Maalim",
"speaker_title": "Hon. Temporary Speaker",
"speaker": {
"id": 16,
"legal_name": "Farah Maalim Mohamed",
"slug": "farah-maalim"
},
"content": " Mhe. wa Kesses, angalia jinsi unavyoweza kuboresha Kauli hii."
},
{
"id": 1560940,
"url": "https://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1560940/?format=api",
"text_counter": 192,
"type": "scene",
"speaker_name": "",
"speaker_title": "",
"speaker": null,
"content": "(Laughter)"
},
{
"id": 1560941,
"url": "https://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1560941/?format=api",
"text_counter": 193,
"type": "speech",
"speaker_name": "Kesses, UDA",
"speaker_title": "Hon. Julius Rutto",
"speaker": null,
"content": " Mhe. Spika wa Muda, unanipatia mtihani mkubwa sana. Wacha niongee kwa lugha ya Kimombo."
}
]
}