GET /api/v0.1/hansard/entries/?format=api&page=154702
HTTP 200 OK
Allow: GET, POST, HEAD, OPTIONS
Content-Type: application/json
Vary: Accept

{
    "count": 1608389,
    "next": "https://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/?format=api&page=154703",
    "previous": "https://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/?format=api&page=154701",
    "results": [
        {
            "id": 1565212,
            "url": "https://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1565212/?format=api",
            "text_counter": 152,
            "type": "speech",
            "speaker_name": "Sen. Mungatana, MGH",
            "speaker_title": "",
            "speaker": null,
            "content": "Jambo la pili na la mwisho kuhusu hizi mimba za mapema, naomba wazazi wawe na muda wa kukaa na watoto wetu. Wakati wanapotoka asubuhi kuenda shambani, kuuza sokoni, kuenda shuleni au kuchunga mbuzi na ng’ombe, wanaporudi jioni, tuchukue nafasi kukaa na watoto wetu. Dunia imechafuka sehemu nyingi ikiwemo kwa mitandao, mazungumzo na hata sehemu ambazo watu wanakunywa pombe. Kwa hivyo, kama wazazi, tuchukue jukumu la kuongea na watoto wetu. Kwa kiingereza tunasema, “ push back”. Kama ilivyosemekana hapa, mimi ni mzazi wa wasichana. Nilidhani kwamba ili watu wafahamiane wanaenda kuongea huku wakinywa chai, kisha baadaye wanaenda kwa mkahawa ama kwa mbuga ya wanyama ama kununua njugu na kukaa chini ya miti. Nilikuwa sijui kwamba siku hizi mambo ni tofauti. Wasichana wangu wamenieleza yale mambo yanayoendelea duniani. Nimeshtuka kujua kwamba siku hizi kila kitu kinafanywa kwa mtandao na sio kama zamani. Wasichana wangu wananieleza ya kwamba hawawezi kuenda kufahamiana na mtu huku wakila njugu. Mambo yamebadilika na sio kama zamani tena. Kwa hivyo, ni lazima tukae na tuwaongeleshe hawa watoto wetu. Hii ni kama vita kwa sababu usipowaongelesha, ukweli wa watoto wako utakuwa ni ukweli wa wale watoto ambao wako na tabia mbaya. Ukweli wa watoto wako itakuwa zile video chafu ambazo wanaangalia katika internet na zile stori wanaambiwa na watu wengine. Lazima tuchukue nafasi ya kupinga kabisa haya mambo na kuwafundisha maadili na dini. Isikuwe kwamba tunawangojea watu wa kanisa ama watu wa madrasa wawafunze dini. Sisi wenyewe kule nyumbani, lazima tukae na kuomba na watoto wetu; tuongee nao na tuwafunze ili mambo haya ya mimba zisizo takikana yapungue. Bw. Spika wa Muda, kati ya mambo mengi ambayo lazima tufanye sisi kama Wakenya, lazima tuchukue majukumu yetu kama wazazi ili kupigana na hizi mimba za mapema. Asante, Bw. Spika wa Muda."
        },
        {
            "id": 1565213,
            "url": "https://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1565213/?format=api",
            "text_counter": 153,
            "type": "speech",
            "speaker_name": "Sen. Murgor",
            "speaker_title": "",
            "speaker": null,
            "content": "Bw. Spika wa Muda, asante kwa kunipa nafasi hii. Mimba za mapema ni kitu ambacho kimeshika mwendo sana siku hizi. Ninaunga mkono yale wenzangu wamesema kwamba umaskini umezidi na ndipo watoto wanajipata tu wanaongozwa kufanya haya maneno kupitia njia ambazo ni rahisi kama kununuliwa switi na biskuti. Vitu kama hivi vinafanya watoto wachukuliwe na watu walio na nia mbaya. Njia ambayo imekuwa rahisi sana ni watu wa pikipiki hasa ambao wanabeba watoto wetu na kuwapeleka shuleni, sokoni ama kuenda pahali ambapo wanataka kuenda. Kuna watu fulani ambao huwa wanajifanya wanawasaidia na hata saa zingine wanawabeba bure bila malipo. Kwa njia hii, wanaweza kulala nao na kuwapachika mimba. Utapata ya kwamba kule nyumbani baba na mama siku hizi hawajali kuketi na watoto wao na kuwaongelesha. Zamani wamama walikuwa wanaongelesha hasa wasichana wale ambao wameanza kupata hedhi. Wamama walikuwa wanajua ya kwamba bila shaka wataweza kupata mimba wakati wowote. Kwa hivyo, walikuwa The electronic version of the Senate Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Director, Hansard and AudioServices, Senate."
        },
        {
            "id": 1565214,
            "url": "https://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1565214/?format=api",
            "text_counter": 154,
            "type": "speech",
            "speaker_name": "Sen. Murgor",
            "speaker_title": "",
            "speaker": null,
            "content": "wanawakaribia kabisa, kuongea nao na kuweka maneno wazi, ili msichana ajue ya kwamba akilala na mwanaume, mimba inaweza kupatikana wakati wowote. Siku hizi wamama wameachia walimu wawe ndio wanakaribia watoto na labda wanawaachia watu wa kanisa ama madrasa waongeleshe watoto. Hata hivyo, hao pia saa zingine wengine huko wanakuwa nyangau ama wale ambao wataweza kutumia hao watoto vibaya. Kwa hivyo, kila pahali sasa ni hatari kwa mtoto msichana na mvulana pia. Hii ni kwa sababu watoto wavulana pia wameingia katika hali hiyo ya kutumiwa vibaya na watu walio na nia mbaya. Ili tuweze kukabiliana na hali ambayo tukonayo sasa ni kuongea na watoto kwa njia ambayo ni wazi. Haswa, baba na mama wenyewe wanastahili waongee kwanza na wajadili juu ya watoto wao na mienendo ya kila mtoto vile anaendelea, ili waweze kuwasaidia wasiweze kutumiwa vibaya na wajikute wako mimba. Mtoto msichana akisha pata mimba ni kama mwisho wa barabara ya maisha yake ya kesho. Hata ingawa tunapiga piga kiraka kidogo, tunasema aache mtoto pahali na arejee shuleni, lakini huyo ni mtu ambaye tayari ameumia na hali yake vile alikuwa huru na aliota ndoto zake za baadaye yanaanza kudimimia na kuwa mtu ambaye amenusirika hali ambayo haiwezi kumuendeleza katika maisha yake. Pia, hii tabia ya wazazi haswa wazee kuingia sana katika mvinyo, inawaweka katika hali ya kutojali. Wao sasa hawaoni watoto wao wanaelekea aje kwa sababu wanaingia nyumbani wakati ambao watoto wamelala. Kwa hivyo, inafaa wazazi wajirekebishe kabisa ili waweze kustahimili yale ambayo yanawakumba watoto wao kwa wakati wa sasa. Asante."
        },
        {
            "id": 1565215,
            "url": "https://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1565215/?format=api",
            "text_counter": 155,
            "type": "speech",
            "speaker_name": "Sen. Abdul Haji",
            "speaker_title": "The Temporary Speaker",
            "speaker": null,
            "content": " Hon. Senators, the time for Statements and contributions to Statements has now lapsed. We will have to proceed to the next Order. At this juncture, I will rearrange the Order Paper, so that we defer Orders No.9 to 14 and proceed to Order No.15. Clerk, next Order."
        },
        {
            "id": 1565216,
            "url": "https://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1565216/?format=api",
            "text_counter": 156,
            "type": "heading",
            "speaker_name": "",
            "speaker_title": "",
            "speaker": null,
            "content": "BILL"
        },
        {
            "id": 1565217,
            "url": "https://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1565217/?format=api",
            "text_counter": 157,
            "type": "scene",
            "speaker_name": "",
            "speaker_title": "",
            "speaker": null,
            "content": "Second Reading"
        },
        {
            "id": 1565218,
            "url": "https://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1565218/?format=api",
            "text_counter": 158,
            "type": "heading",
            "speaker_name": "",
            "speaker_title": "",
            "speaker": null,
            "content": "THE PROVISION OF SANITARY TOWELS BILL (SENATE BILLS NO.7 OF 2024)"
        },
        {
            "id": 1565219,
            "url": "https://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1565219/?format=api",
            "text_counter": 159,
            "type": "scene",
            "speaker_name": "",
            "speaker_title": "",
            "speaker": null,
            "content": "(Bill deferred)"
        },
        {
            "id": 1565220,
            "url": "https://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1565220/?format=api",
            "text_counter": 160,
            "type": "heading",
            "speaker_name": "",
            "speaker_title": "",
            "speaker": null,
            "content": "BILL"
        },
        {
            "id": 1565221,
            "url": "https://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1565221/?format=api",
            "text_counter": 161,
            "type": "scene",
            "speaker_name": "",
            "speaker_title": "",
            "speaker": null,
            "content": "Second Reading"
        }
    ]
}