2 Apr 2025 in Senate:
Asante, Bw. Spika. Swali langu linahusu muda. Bw. Waziri, waswahili husema, mnyonge mnyongeni na haki yake mpe. Umesema ya kwamba kuna mazungumzo ambayo yanaendelea ili kuhakikisha kwamba wale ambao hawakulipwa pesa zao waweze kuzipata. Ukipiga hesabu, utapata ya kwamba takriban miaka 27 zimeisha. Wengi wao walikufa wakingojea pesa zao. Bw. Waziri, ingekuwa wewe, ungeweza kungoja pesa kwa miaka karibu 30 ilhali uko na matumizi ya hizo pesa? Je, inawezekana utupe muda ambao unaona kama unakadiria? Hili jambo linaweza kumaliziwa ili hawa watu waweze kufaidika na pia waweze kupata nafuu kwa sababu pesa zao zimekaa kwa muda mrefu sana. Nchi hii ...
view
2 Apr 2025 in Senate:
Asante sana, Mstahiki Spika, kwa kunipa nafasi kuchangia na kutoa tafsida yangu kwa Taarifa iliyoletwa na Sen. Orwoba. Wakati huu nchi inapambana kuhakikisha kwamba vijana na wananchi kwa jumla wanapata kazi hapa na nchi za nje. Ni jambo la aibu kuona watu wakiritimba wamejipanga kuhadaa Wakenya. Hakuna jambo mbaya kama mawakala tisa wameungana na benki tatu kuhakikisha kwamba wamewalaghai wanaotafuta kazi. Waziri wa Leba na Maslahi ya Jamii anafaa kujua mambo haya yote kabla hayajafika hapa. Kama amemakinika anafaa kujua kuna jambo linaendelea kule nje na Wakenya wanapoteza fedha zao. Bwana Spika, mambo ni wawili- iwe anafahamu kinachoendelea au la. ...
view
2 Apr 2025 in Senate:
Tunao ushahidi ni akina nani wanafanya mambo hayo. Tunajua inaendelezwa katika ofisi zipi. Wanaotenda hayo wanafanya sinema ya Kichina kutuonyesha wanavyopeleka watu nchi za nje. Watoto wetu bado wako kule mashinani na pesa zao zimepotea. Benki inaitisha Shilingi 5,000 kutoa mkopo ili ilipe moja kwa moja kwa wale mawakala bila kupitia kwa wale wanaotafuta kazi. Imefika wakati ambao sisi kama Seneti tunafaa kusimama tusichukuliwe kama wanasesere kwa sababu tunajua tunayofanya.
view
2 Apr 2025 in Senate:
Asante sana, Mstahiki Spika. Kwanza nikushukuru kwa swali ambalo umeuliza kuhusu vyama vya ushirika kufilisika. Jambo la kwanza, sababu kubwa huwa uongozi mbaya kwa vyama vya ushirika na wale wanaoongoza vyama vile kule mashinani. Bw. Waziri, unajua tukianza kutatua tatizo, lazima tuweke msingi. Kulikuwa na sababu kubwa ambayo ilifanya Kimuri kufilisika. Inafaa kuangaliwa kwa kina ilifisika kwa nini. Tunapojaribu kuongeza kuzalisha kahawa, na wakulima bado wanaenda kilomita 10 kupeleka kahawa kwa mitambo ya kusagia, wengi wataenda kulima vitu mimmea nyingine ambayo haina maana kushinda kahawa. Kitu ambacho ningeambia Bw. Waziri ni kwamba chanzo kubwa ya kufilisika kwa vyama vya ushirika ...
view
2 Apr 2025 in Senate:
kujiuzia wenyewe. Mahali tumepitia, Bw. Waziri Mbadi anataka kukula kutoka kwa kikapu chetu. Aangalia hilo, Bw. Waziri.
view
2 Apr 2025 in Senate:
On a point of clarification, Madam Temporary Speaker.
view
2 Apr 2025 in Senate:
Asante, Bi. Spika wa Muda. Bw. Waziri, sijui unafahamu kwamba kina Cheskaki na Cheptai’s wa Bungoma mwaka huu wamepata shilling 51 tu kwa kilo ya kahawa. Nimekusikia ukisema ya kwamba wakulima sasa hivi wanalipwa shilingi 100 na zaidi. Kahawa ya watu wa Bungoma imeuzwa kwa shilingi 100 tu kwa kilo moja, Bw. Waziri. Kwa hiyo, siyo ukweli. Kuna wakulima hawajanufaika na jitihada mnazofanya kama Serikali ama Wizara kupata bei nzuri ya kahawa.
view
27 Mar 2025 in Senate:
Asante sana, Bw. Spika. Ningetaka kwanza kushukuru Kamati ya Fedha na Bajeti kwa kazi nzuri waliofanya. Ningependa kusema ya kwamba adui mkubwa wa ugatuzi ni wale walio katika Bunge la Kitaifa. Mswahili husema ya kwamba ukibebacho ukivuja, nafuu kwa mchukuzi. Uongozi wa Bunge la Kitaifa unafaa kumakinika na kuhakikisha ya kwamba hakuna vuta nikuvute tunapopitisha Mswada. Hii ni kwa sababu sisi ndio walinzi wa The electronic version of the Senate Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Director, Hansard and AudioServices, Senate.
view
27 Mar 2025 in Senate:
ugatuzi. Pesa ambazo zinaenda kwa kaunti hazikuji kwetu kama Maseneta. Pesa hizo zinaenda kufaidi Wakenya. Kwa hivyo, ningetaka kuwasuta kwa hilo na kuwaambia ya kwamba miwa ukipewa kibogoyo mzee kama zawadi, inakuwa ni matusi. Pesa tunazopitisha siku ya leo zimecheleweshwa kwa sababu ya vuta nikuvute ambayo haina maana. Tunafuraha kwa sababu maafisa ambao wanafanya kazi ngumu katika gatuzi zetu watapata pesa zao. Naona Kirinyaga wako na Shilingi 6,000,000. Hakukuwa na maana yoyote ya kuchelewa kulipa wafanyikazi hao kiwango hicho ilhali wanafanya kazi ngumu kule mashinani. Wengi wao wanaenda kazini wakitembea kama mawakala wa ng’ombe. Wengine hawana hata usafiri ya kuhakikisha ...
view
12 Mar 2025 in Senate:
Bw. Spika, nadhani Waziri anaweza kujibu swali langu kwa sababu ni jambo ambalo limekuwa likisumbua watu wengi. Mnamo tarehe moja mwaka wa 2023, WRA iliongeza bei ya maji kwa wakulima na watu wengine. Mwezi wa saba mwaka wa 2023, kulikuwa na agizo la mahakama ambalo lilisimamisha watu ambao wanatumia maji kufanya ukulima na kunywa kulipishwa kodi mpaka kesi itakaposikilizwa. Je, kwa nini mpaka sasa hivi wananchi wa Kenya wanaendelea kulipishwa maji ambapo bei iliongezwa kutoka thumuni hadi shilingi tano kwa kila lita elfu moja ilhali kuna agizo la mahakama?
view