Ali Menza Mbogo

Parties & Coalitions

All parliamentary appearances

Entries 21 to 30 of 292.

  • 15 Oct 2024 in National Assembly: pia wapewe fedha wafanye miradi pamoja na serikali za ugatuzi ili watu wetu waweze kuendelea haraka na sehemu zilizobaki nyumba ziweze kuendelea kwa kasi. Hivi sasa, hali ya uchumi ni ngumu sana lakini itakapokuwa sawa, ni muhimu fedha zaidi zifike mashinani. Utulivu ulioko katika taifa umeletwa na serikali za ugatuzi. Angalau watu wanapata vibarua. Mpango wa kazi kwa vijana unatoa ajira kwa miezi miwili au mitatu, na vijana wanajisaidia. Vijana wanapokosa fedha, mambo yote yanakuwa magumu. Katika Serikali kuu, tatizo ni kwamba mambo mengi hufanywa kwa msingi wa ukabila na kuleta hali ya sintofahamu. Nimesimama hapa kusema kwamba tukubaliana kwamba ... view
  • 15 Oct 2024 in National Assembly: Ahsante sana Naibu Spika wa Muda kwa kunipatia fursa ya kuchangia ubora wa chakula ama ulinzi wa chakula bora mpaka ufikie mnunuzi. The electronic version of the Official Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Hansard Editor. view
  • 15 Oct 2024 in National Assembly: Ni muhimu kuwe na taratibu ya vipi tutalinda chakula kuanzia pale shambani kwa hali ya ubora mpaka ifike sokoni, mahali ambapo kuna ununuzi unayofanywa kwa mazingira mazuri. Taifa ambalo liko na nguvu au liko na maendeleo ni lile ambalo watu wake wako na afya. Mara nyingi, afya hutokana na matumizi ya vyakula ambavyo wanavitumia na haswa, upandaji kuanzia shambani hadi sokoni. view
  • 15 Oct 2024 in National Assembly: Mheshimiwa Spika wa Muda, taifa letu sasa limekumbwa na maradhi ya saratani. Kumekuwa na kesi nyingi za saratani mpaka hata watoto wadogo wako na saratani. Kwa sababu ya umaskini, watu wetu wengi wanapoteza maisha yao majumbani mwao kwa sababu hawana uwezo wa kwenda hospitali kutibiwa. Wale wanaokwenda ni wale wanaojiweza. Ukienda pale, inakuwa ni vigumu sana kupata matibabu kama huna fedha. Ijapokuwa hospitali ni za Serikali, bei ya matibabu ni ghali mpaka hata mtu haziwezi kulipa kama hana kazi au bima. Hivi sasa, idadi kubwa ya Wakenya hawana kazi na kwa hivyo, wanapopatwa na maradhi kama hayo, inakuwa hali ni ... view
  • 15 Oct 2024 in National Assembly: Nitakupa mfano, Mheshimiwa Spika wa Muda. Kuku wa gredi hupewa kemikali ili wazidi kufura. Vifurushi vya kemikali hizo vimeelezea kuwa baada ya kuku hao hupewa kemikali hizo, wasitumike kama chakula kwa siku kadhaa mpaka ile sumu itoke miilini mwao. Lakini kwa sababu Shirika la Viwango halijali Wakenya, wale kuku wanaopewa zile dawa, kesho wanapatikana kwenye soko. Mtu anamnunua kuku amechomwa, anamla kisha inamdhuru baada ya masiku kadhaa. Anapopimwa wakati wa matibabu, anaambiwa kuwa anaugua saratani. Tayari taifa letu lina gharama kubwa ya kupeleka madawa hospitalini. Wangelizuia gharama hiyo ikiwa wangeangalia sehemu ambapo nyama hiyo inatoka. Wangelichunguza ni mbolea gani inatumiwa ... view
  • 15 Oct 2024 in National Assembly: Kwa hivyo,, ni sawa kukiwa na utaratibu wa kuwalinda wananchi kwa sababu wanalipa ushuru wakitegemea kuwa Serikali ina Shirika la Viwango. Wao hawajui ni kitu gani kinachoendelea. Mboga zinazopandwa mashambani, zinanyunyiziwa kemikali fulani ambayo pia inatakikana kukaa kwa muda fulani. Kemikali hiyo inafanya jani liwe kubwa kwa haraka na wakati huo huo, mboga zinatolewa shambani na kupelekwa sokoni ambapo mwananchi wa kawaida anauziwa. Unapata watoto wako na vitumbo vikubwa unafikiria kuwa wameshiba ilhali ni maradhi tu. Yote yanasababishwa na Shirika la Viwango katika Kenya. Kwa hivyo, kama Shirika hilo halina wafanyikazi wa kutosha, waseme hivyo. Hawana view
  • 15 Oct 2024 in National Assembly: ya kutosha ili watembee katika mashamba kukagua mifugo wanapokamuliwa na kuhakikisha kuwa wanakamuliwa katika mazingira mazuri. Isiwe kuwa mifugo hao wanakamuliwa na watu wamejaa matope kisha maziwa hayo yanapelekwa mahali ambapo yanauzwa. Lazima kuwe na utaratibu wa kumlinda mwananchi ili awe na uhakika. Hata watalii wakija hapa nchini na wakule vyakula bora, hiyo ni mojawapo ya njia za kuwavutia. Wanajua kuwa ukitaka kula vyakula bora, nenda Kenya. Lakini ikiwa hatutakuwa tumejipanga vizuri, basi mambo mengi yataharibika na maradhi yatakuwa mengi. view
  • 15 Oct 2024 in National Assembly: Kwa hivyo, Mheshimiwa Spika wa Muda, nimesimama… view
  • 15 Oct 2024 in National Assembly: Niko sawa. view
  • 25 Sep 2024 in National Assembly: Asante sana, Mhe. Spika wa Muda, kwa kunipatia fursa ili nichangie Hoja hii muhimu sana kuhusu elimu. Kwanza, ninampongeza Mhe. Passaris kwa kuileta hapa ili watoto wote wapate elimu ya bure. Lakini, ninataka kukosoa ule mfumo ambao anautaka. Haya mambo yamejaribiwa katika taifa hili; kuwa na mfuko moja katika kila sehemu. Hii imesababisha kuzorota kwa taifa zima. Katika sehemu zingine unaskia wakisema wako nyuma ilhali wengine wako mbele. Hii ni kwa sababu ya mfumo wa zile fedha kuwa katika sehemu moja halafu zinagawanywa vile wanavyotaka wao - kisiasa na kwa njia isio sawa. Ikiwa pesa zitaenda mashinani, kila sehemu itapata ... view

Comments

(For newest comments first please choose 'Newest' from the 'Discussion' tab below.)
comments powered by Disqus