Ali Menza Mbogo

Parties & Coalitions

All parliamentary appearances

Entries 31 to 40 of 169.

  • 19 Apr 2023 in National Assembly: shida kubwa sana ya ukosefu wa ajira kwa vijana. Kwingine, bodaboda hututumika kama ambulensi za kubebea wangonjwa, haswa sehemu ambazo barabara ni mbaya. Kwa hivyo, view
  • 19 Apr 2023 in National Assembly: ni sekta muhimu ambayo inapaswa kuboreshwa. Ni kweli kuwa kuna ajali nyingi sana zinazosababishwa na bodaboda . Kama wenzangu walivyosema, katika hospitali nyingi, kuna wodi zilizotengewa watu wa bodaboda tu kwa sababu ni wengi. Hii inasababishwa na kutokuwa na mafunzo ya uendeshaji wa bodaboda hizo. Sekta hii pia inashuhudia umaskini mwingi sana. Maskini wengi sana ndio wanatumia mfumo huu wa usafiri. Wengi wa waendeshaji wanashindwa kwenda kusomea uendeshaji wa view
  • 19 Apr 2023 in National Assembly: kwa sababu ya bei ghali ya karo. Tunapaswa kubuni taratibu zinazofanya bei ya karo kuwa tahafifu ili waendeshaji bodaboda waweze kwenda shule na kujua kanuni za barabara. Wengi wanashindwa kwenda kusoma kwa sababu hali ni ngumu. Pia wanatakiwa kupatia wenye bodaboda Ksh500 kwa siku, kwa kila Ksh1,000 wanazopata. Kwa hivyo, tunapaswa kubuni taratibu zitakazofanya bei ya karo iwe tahafifu ili waendeshaji bodaboda wapate mafunzo na ujuzi wa kuendeleza biashara hii. view
  • 19 Apr 2023 in National Assembly: na tuk-tuk ni muhimu sana. Kwa hivyo, kama Bunge la Taifa, tunapaswa kubuni taratibu za kuwasaidia. Hata serikali za ugatuzi zinapaswa kutoa viegezo vya kujikinga haswa wakati kama huu wa mvua na pia wakati wa jua. Serikali za kaunti pia ziwapatie helmets na pia sehemu za kusafisha helmets hizo. Si tu watu kutumia helmets na koti zile bila kusafishwa. Zinaweza kusababisha maradhi. Ni mambo mengi ambayo tunahitaji kupanga kwa utaratibu ili kukuza sekta hii ili iweze kuwafaidisha watoto na vijana wetu. view
  • 19 Apr 2023 in National Assembly: Mhe. Spika wa Muda, sitazungumza mengi zaidi. Nakushukuru kwa kunipatia nafasi. Imebaki siku moja au mbili kufikia sikukuu yetu na nawatakia Waislamu wote sikukuu njema. Mungu awabariki, Insha Allah . view
  • 16 Mar 2023 in National Assembly: Asante sana Mhe. Spika wa Muda kwa kunipa fursa ili nipenyeze sauti yangu. Ningependa kuchukua nafasi kumpongeza Mwenyekiti wa Hazina ya Maeneo Bunge kwa kuleta majina ya maeneo Bunge matatu ili yaweze kupitishwa. Ni vizuri sana yapitishwe kwa sabau kuna shida kubwa sana mashinani. Watoto wengi hawaendi shule kwa sababu hawana karo. Shida zimekuwa nyingi. Kwa hivyo haya maeneo Bunge matatu ambayo majina yao hayajakuja yako katika shida kubwa sana. Naomba sisi sote tushirikiane kuhakikisha kwamba haya majina yamekuwa Gazzeted mapema sana kwa sababu hali ni nzito. Pia, ningependa nichukue fursa hii kumweleza mwenyekiti wa hazina hiyo kwamba ni muhimu ... view
  • 16 Mar 2023 in National Assembly: . Shida ni kubwa ndugu yangu mwenyekiti. Naomba uwasukume kwa sababu katika ahadi walizotoa tukiwa Pride Inn ni kwamba kila wiki mbili watatoa shilingi bilioni nne. Baada ya hapo hakuna kitu tumeona, hata ndururu! Hali ni ngumu sana. Watoto wa university hawaendi shule kwa sababu ya hali ngumu ya kimaisha. Pia nikutahabarishe Mwenyekiti kwamba Board ya NG-CDF ndiyo inaotoa maamuzi ni kitu gani kifanywe katika maeneo Bunge. Wananchi wamekuwa wakikusanyika wakitoa maamuzi. Kama eneo langu kuna uzoroto wa usalama. Sasa watu wanataka securitylights. Tumekubali tuweke security lights. Ikifikia hapo kwa bodi, wanasema haiwezekani ilhali watu wanaumia. Sio wao wako kule ... view
  • 1 Mar 2023 in National Assembly: Ahsante sana Mhe. Spika wa Muda, kwa kuniruhusu niweze kupenyeza sauti yangu kwa suala hili. Nitafanya haraka kwa sababu ya muda ili wengine wapate nafasi ya kuchangia. Kwa kweli, inasikitisha sana Mahakama Kuu kuidhinisha kusajiliwa kwa vyama hivi vya usagaji na ushoga ama uhanithi. Mimi nitawasihi majaji hao wamche Mwenyezi Mungu. Hapa duniani tumekuja kulima shamba ambalo matunda yake tutayapata mbeleni. Kwa hivyo, lolote wanalolifanya na maamuzi yote wanayoyatoa hivi sasa watakutana nayo mbele akhera, ambapo wote wataondoka katika ulimwengu huu. Hakuna mtu atabaki. Pia wajue kwamba wataweka kumbukumbu za vizazi vilivyoko na vitakavyokuja kulingana na maamuzi ambayo wanayafanya sasa. ... view
  • 21 Feb 2023 in National Assembly: Ninakushukuru kwa taratibu. The electronic version of the Official Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Hansard Editor. view
  • 21 Feb 2023 in National Assembly: Kuhusu swala la CBC, kwa kweli taifa halijakuwa tayari kwa haya mageuzi ya elimu. Shule zilizochaguliwa kuwa na junior secondary school ni chache ukilinganisha na wanafunzi walio wengi zaidi. Walimu waliochaguliwa ni wachache ukilinganisha na shule na wanafunzi. Fedha, pia, za kuwezesha mchakato huu kuendelea kikamilifu. Shule zote hazina mahabara na CBC haiwezikukamilika bila mahabara. Wazazi wanaumia kifedha kupeleka watoto wao junior secondary schools. Wanaambiwa wabadili sare za shule na pia waende na madawati. Kila siku kuna mambo mapya mpaka inakuwa vigumu kutekeleza swala hili. Kwa hivyo, ninasimama na wengi wa Wajumbe Bungeni ambao wamezungumzia kuwa swala hilo bado; Serikali ... view

Comments

(For newest comments first please choose 'Newest' from the 'Discussion' tab below.)
comments powered by Disqus