Parties & Coalitions

All parliamentary appearances

Entries 341 to 350 of 801.

  • 7 Dec 2023 in Senate: (c) Statement sought by Sen. Raphael Chimera, MP, regarding the adherence to principle of meritocracy, transparency, fairness and equal opportunity in recruitment at the Competition Authority of Kenya (CAK), particularly in recruitment of the Director General of the Authority. Mr. Deputy Speaker, Sir, the Committee considered responses for Statements and will conclude the report soon after appearance of stakeholders who have already been invited by the Committee. The Committee held a joint sitting with the Standing Committee on National Security, Defence and Foreign Relations, Standing Committee on Land Affairs and Human Rights on 14th September, 2023, with the National Steering ... view
  • 7 Dec 2023 in Senate: (c) Statement sought by Sen. Raphael Chimera, MP, regarding the adherence to principle of meritocracy, transparency, fairness and equal opportunity in recruitment at the Competition Authority of Kenya (CAK), particularly in recruitment of the Director General of the Authority. Mr. Deputy Speaker, Sir, the Committee considered responses for Statements and will conclude the report soon after appearance of stakeholders who have already been invited by the Committee. The Committee held a joint sitting with the Standing Committee on National Security, Defence and Foreign Relations, Standing Committee on Land Affairs and Human Rights on 14th September, 2023, with the National Steering ... view
  • 6 Dec 2023 in Senate: Asante, Bw. Spika, kwa nafasi hii ili nijiunge na wenzangu kuzungumza juu ya shida za Bunge la Seneti. Mimi natoka Kaunti ya Marsabit. Juzi tulimsikia Sen. Lomenen wa Kaunti ya Turkana akisema tukienda kipindi cha mapumziko wakati huu, sisi ambao tunawakilisha kaunti hizo hatuna mapumziko. Tunasikia milio ya bunduki ikipigwa kila mahali. view
  • 6 Dec 2023 in Senate: Kaunti ya Marsabit imefurika maji hata watu wameshindwa kufika katika vituo vya chakula. Kwa sasa, tunasaidiwa na helikopta kusambaza chakula. Hata hivyo, Serikali haina helikopta za kutosha. Tuko na shida. Watu ambao wanafanya kazi katika ofisi zetu, hawapati chakula kwa sababu wengi wao wanaishi sehemu ambayo helikopta haiwezi kufika. Wale ambao wanaishi vijijini hawawezi kufika katika vituo vya chakula. Mpaka sasa, wafanya kazi katika ofisi zetu hatujapata pesa za kusimamia shughuli za ofisi hizo. view
  • 6 Dec 2023 in Senate: Safari ya kutoka Nairobi hadi Marsabit ni mbali na gharama ya kusafirisha vitu ni kubwa sana. Watu wetu wana shida ni nyingi sana. Masomo ni duni na kupata chakula ni shida. Ukisikia mtu katika Kaunti ya Nairobi akisema anaumia mara 10, basi sisi tunaumia mara 100 kwa sababu ya shida za usafiri na milio ya risasi. Kiangazi kikija, kinakithiri. Pia mvua ikinyesha, inakithiri, mafuriko yanakuja na milio ya bunduki ni kila mahali. view
  • 6 Dec 2023 in Senate: The electronic version of the Senate Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Director, Hansard and AudioServices, Senate. view
  • 6 Dec 2023 in Senate: Kwa hivyo, tukienda mapumziko kesho, mimi sijui kama nitaenda Marsabit. Kama watu hao wangepata hizo pesa, wangenunulia familia zao chakula. Watu wetu hawana chakula na wanaendele kuteseka. Sisi tuna shida nyingi sana ingawa tuko katika Serikali moja. Hata ukiwa upande wa Upinzani au Serikali, sisi sote tunahudumia nchi moja, wananchi wetu na familia zetu. Jana Wabunge wa Bunge la Kitaifa walisusia kazi lakini leo wamerudi kwa sababu watalipwa marupurupu yao ya National Government Constituencies Development Fund (NG-CDF). Mimi naona kama hili Bunge la Seneti tunaonyeshwa kwamba halina maana katika nchi hii. Ni mara ngapi Mawaziri wamekataa kuja hapa wakisema wanaugua, ... view
  • 6 Dec 2023 in Senate: Jana niliona maajabu sana katika mtandao wa Twitter na nilishangaa sana. Kuna wageni kutoka Somaliland ambao walikuja kwa Ofisi ya Spika wa Seneti. Mhe. Spika aliwakaribisha na mimi pia nilikuwa hapo. Msimamizi wa Somaliland alisema kuna takriban Wakenya 30,000 wanafanya kazi Hargeisa huko Somaliland. Akaongezea kusema kuna wanakandarasi wa Kenya ambao wamejaa huko. Alieleza kwamba hawana mayai wala kuku huko Somaliland. Mayai na kuku ambao wanakula wanatoka Uropa. view
  • 6 Dec 2023 in Senate: Akasema pia majani chai ambayo yangetoka Kenya yaende moja kwa moja hadi Somaliland, yanaenda Uropa na Uturuki ndio irudishwe Somaliland. Hayo majani chai ni ya wakulima wetu ambayo yanapelekwa huko Uropa na Uturuki kisha yanauzwa katika Somaliland. Huyo msimamizi aliiomba Serikali ya Kenya ianzishe huduma za usafiri wa ndege kutoka Nairobi hadi Hargeisa, Somaliland. Hiyo safari itarahisisha maisha ya watu wanaosafiri kikazi kutoka Kenya hadi Somaliland. Wale wanaoishi Somaliland, pia wakaomba huduma ya ndege kati ya Hargeisa na Nairobi. view
  • 6 Dec 2023 in Senate: Alizidi kusema ya kwamba imechukua miezi 18 na mpaka sasa, hawajapata huduma za usafiri wa ndege kwenda mpaka Hargeisa. Nakumbuka alisema wanaenda Hargeisa kupitia Djibouti ama Ethiopia na gharama yake ni takriban Dola 1,800. view

Comments

(For newest comments first please choose 'Newest' from the 'Discussion' tab below.)
comments powered by Disqus