Mohamed Faki Mwinyihaji

Parties & Coalitions

All parliamentary appearances

Entries 1861 to 1870 of 2095.

  • 18 Jun 2019 in Senate: Juzi, Kamati ya CPAIC ilizuru Kaunti ya Samburu, ambako tulipata miradi mingi imekwama kwa sababu ya ukosefu wa fedha, ilhali kila mwaka tunaomba fedha za kuendesha miradi hii. Kila mwaka, watu wanatengeneza Annual Development Plans (ADP) ili kusaidia kutekeleza Vision 2030, ambayo ni ramani inayotumika na Serikali kuhakikisha tunapata maendeleo nchini. Kila miradi inapokwama, maendeleo yanabaki nyuma, na Serikali inashindwa kufikia Millennium Development Goals (MDGs), ambazo zimekwama katika Ruwaza ya 2030 katika mwongozo wa miradi ya Serikali. Ni muhimu kabla ya miradi mipya kuzinduliwa, ile iliyopangwa kufanyika katika mwaka fulani wa fedha za serikali ikamilishwe. La sivyo, ni muhimu kuweka ... view
  • 18 Jun 2019 in Senate: Bi. Spika wa Muda, Wabunge au magavana pia wanabagua sehemu ambazo hazikuwapigia kura. Utapata sehemu zilizopigia kiongozi fulani kura kwa wingi zinapelekewa miradi kwa wingi, na kule kwingine hakupati miradi yoyote. Kwa hivyo, jambo hili linasababisha kutokuwa na usawa wa maendeleo katika sehemu tofauti za kaunti moja. Kwa hivyo, hili ni donda sugu. Ni lazima tutafute njia mwafaka ya kuhakikisha kwamba miradi inakamilishwa kwanza kabla ya kuanzishwa miradi mipya na serikali za kaunti au Serikali Kuu. Vile vile, lazima maendeleo yasambazwe katika maeneo yote katika kaunti ama nchi kwa usawa, kwa sababu sote tunalipa kodi katika mfuko mmoja. Haiwezekani kwamba ... view
  • 18 Jun 2019 in Senate: Nikimalizia, hii miradi lazima ikamilishwe kwa wakati unaofaa ndio wananchi wafaidike na miradi iliyonuiwa kufanyika. view
  • 18 Jun 2019 in Senate: Naunga mkono Mswada wa Sen. Kibiru. view
  • 13 Jun 2019 in Senate: Asante sana, Bi. Spika wa Muda, kwa kunipa fursa hii kuchangia taarifa ya Seneta wa Kaunti ya Kericho, Sen. Cheruiyot. Maswala ya pasipoti imekuwa donda sugu kwa wakaazi wa pwani kwa jumla hususan wale waumini wa dini ya Kislamu. Sheria inayotumika kuwapa Waislamu pasipoti ni tofauti na sheria inayotumika kuangalia maombi ya pasipoti ya Wakenya wengine. view
  • 13 Jun 2019 in Senate: Hivi majuzi tulikuwa na mchakato wa kuandikisha Huduma Namba. Stakabadhi zilizokuwa zinahitajika kuandikisha Huduma Namba zilikuwa kadi ya kitambulisho au cheti cha kuzaliwa pekee lakini kupata pasipoti, unahitajika kuleta vyeti vya kuzaliwa za babu na babu. view
  • 13 Jun 2019 in Senate: Babu yangu alipozaliwa, Kenya haikuwa imepata uhuru. Kenya ilipata uhuru mwaka wa 1963. Kwa hivyo, sitapata cheti cha kuzaliwa cha babu yangu kuonyesha kwamba yeye ni Mkenya kwa sababu Kenya haikuwa imepata uhuru alipozaliwa. Donda sugu la pasipoti limekuwa likiwapa Wakenya wengi hususan wale wa kaunti ya Mombasa na miji mingine ya pwani shida kubwa. view
  • 13 Jun 2019 in Senate: Bi. Spika wa Muda, maeneo mengine penye ofisi za pasipoti ni kama Kisumu, Nakuru, Kisii, Embu na maeneo mengine ambapo mwendo ni kama kilomita 100 au 50 kutoka Nairobi. Wale wanaohitaji huduma hizi kwa wingi wamenyimwa nafasi za kuwa na pasipoti. Kwa mfano, pwani nzima, ofisi ya paspoti ni moja tu mjini Mombasa. view
  • 13 Jun 2019 in Senate: Naunga mkono taarifa hii ili tuhakikishe Wakenya wanaweza kupata pasipoti kwa njia rahisi. Nafasi za kazi hapa Kenya ni adimu, kwa hivyo wengi wakiwa na pasipoti, wataweza kuenda kufanya kazi katika nchi zingine ili waweze kujielendesha kimaisha. Ikiwezekana, Kamati husika inafaa kutembelea ofisi za pasipoti ili wajionee shida zinazowakumba Wakenya. view
  • 13 Jun 2019 in Senate: Bi. Spika wa Muda, Wakenya wengine wenye dini ya Kiislamu huambiwa kwamba lazima wafanyiwe vetting . Hakuna sheria inayosema kwamba lazima mtu afanyiwe vetting ndipo aweze kupata pasipoti. Ikiwa mtu ana kitambulisho au cheti cha kuzaliwa, hafai kufanyiwa vetting anapotafuta paspoti. view

Comments

(For newest comments first please choose 'Newest' from the 'Discussion' tab below.)
comments powered by Disqus